logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matamshi ya Muturi dhidi ya Ruto yalitokana na kupoteza kazi serikalini - Isaac Mwaura

Msemaji wa serikali Isaac Mwaura alisema kuwa matamshi ya Muturi kwa Rais ni kutokana na hasira ya kupoteza kazi

image
na Evans Omoto

Yanayojiri07 April 2025 - 10:24

Muhtasari


  • Alielezea kuwa Bwana Muturi aliendeleza msururu wa mashambuzi ya maneno kuelekezwa  kwa rais kwa sababu hayuko ndani ya serikali.

Isaac Mwaura Msemaji wa serikali

Msemaji wa serikali Bwana Isaac Mwaura alisema kuwa matamshi yake aliyekuwa waziri wa utumishi wa umma Justine Muturi ni kutokana na hasira ya kupoteza ajira.

Alisema hayo alipokuwa akihojiwa na  runinga ya NTV Jumatatu asubuhi ambapo alielezea kuwa Bwana Muturi aliendeleza msururu wa mashambuzi ya maneno kuelekezwa  kwa rais kwa sababu hayuko ndani ya serikali.

Bwana mwaura alisema kuwa iwapo una  mambo ambayo hayakufurahishi katika serikali unalistahili kuelezea malalamishi yako ndani ya vikao vya baraza la mawaziri ambalo huongozwa  na rais .

 Kwa kufanya hivyo ungekuwa  unatiii na kuheshimu hatikiapo ya kulinda na kuheshimmu katiba ya taifa, bali sio kuishutumu serikali na  ilihali upo ndani yake.

''Ikiwa wewe ni kiongozi na unaifanyia serikali kazi hupingi  serikali  hiyo moja kwa moja la hasha kuna vikao vya  baraza la mawaziri ambapo masuala ya ndani huweza kuzungumziwa na  kama kuna shida au tofauti  hapo ndio mahali pema pa kujielezea  si nje'' bwana Mwaura  alisema.

'' ikiwa kwa namna moja au nyigine   ujikute au ipatikane kuwa hupendezwi na sera  za baadhi ya viongozi au jambo  linalozungumziwa hukubaliani nalo hustahiki kutoka nje  na kuanza kuzungumzia tukio bali njia sawa ni kuhakikisha kuwa unajiuzulu kutoka mamlakani, na watu wengi wamefanya hivyo siku za awali.

Kuhusu suala la maendeleo katika sehemu zote za  taifa ambapo wanahabari walitaka kujua ni jinsi  gani maendeleo huweza kusambazwa kote nchini.

Mwaura alisema kuwa kuhusu suala la maendeleo, raisi huweza kuwa na timu yake ya ukaguzi wakiwemo makatibu wake  ambao huzunguka na  kuweka miradi maalum  kipaumbele ili kuhakikisha kuwa miradi ambayo ina umuhimu inshugulikiwa mbele kabla.

Vilevile aliweza kuulizwa kuhusiana na matamshi ya Bwana Muturi kuwa mawaziri huwa wanatishwa na  usimamizi  kauli ambayo  alikanusha kwa kusema kuwa Ruto ni kiongozi mwenye  maamuzi mapevu na huhakikisha kuwa kila mtu anapewa  nafasi ya kujieleza bila kushututishwa.

Vilevile  aliweza kusema kuwa kutokana na mikakati na mienendo ya rais  ya  madili  kuwa rais hana uwezo wa kuongoza taifa kutokana na makosa ya kukisiwa kuwa yeye mi mfisadi alikanusha  kwa kusema huo ni uongo rais  ana historia pana  ya uongozi bora tena wa kuaminika vyema  bwana Mwaura alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved