logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ukosoaji wa Gachagua kwa serikali wazidi kupamba moto

Alityekuwa Naibu wa rais bwana Rigathi Gachagua asisitiza kuwa yungalili imara licha ya kutendewa madhila mengi .

image
na Evans Omoto

Yanayojiri07 April 2025 - 12:23

Muhtasari


  • Bwana Rigathi aliendeleza msusru wa kuikosoa  serikali huku akionyesha msimamo wake kwa watu  wa Kenya  pamoja na kwa watu wa Mlima Kenya  Kuwashiria kuwa hawatishiki wala kubabaika na ziara ya rais Eneo hilo.''
  • Taifa letu haliwezi likaongozwa na na watu wachache au kundi fulani kwa  malengo yao  ya binafsi na vilevile taifa  liliojaa misingi mibovu ya sheria kwa kukosa utaratibu  unaofaa  kwa kufuata sheria'' Gachagua alisema.

Rigathi Gachua aliyekuwa naibu wa rais

Aliyekuwa Naibu wa rais  Rigathi Gachagua  anaonekana kusisitiza kuwa angali imara licha ya kutendewa madhila mengi.

Bwana Rigathi aliendeleza msururu wa kuikosoa  serikali huku akionyesha msimamo wake kwa watu  wa Kenya  pamoja na kwa watu wa Mlima Kenya  Kuwashiria kuwa hawatishiki wala kubabaika na ziara ya rais Eneo hilo.

Akichapisha  katika  mtandao wake wa X, Gachagua aliweza kuandika kwa  kusema,"  .''Kama taifa tunahitaji makuu sio masuala ya kuchochewa na serikali ya vita, sio uchumi ulioangamizwa wala sio  ufisadi, sio  idara za eilimu ambazo hazifanyi  kazi, sio tasisi za  afya ambazo hazifanyi kazi wala sio kuwanyima watu uhuru ambao upo katika katiba na mauaji ya kinyama ya  vijana wetu na vile  uhusiano mbaya wa kidiplomasia  na vilevile  sera mbovu za kimataifa za nje'' Gachagua aliandika katika mtandao wake.

Aliweza kusema kuwa Kama taifa hatuwezi salia katika giza la kuweza kuongozwa kwa kutumia uongozi wa kiimla  na wenye nguvu kwa  kulazimishiwa mambo hapa na pale.

''Taifa letu haliwezi likaongozwa na na watu wachache au kundi fulani kwa  malengo yao  ya binafsi na vilevile taifa  liliojaa misingi mibovu ya sheria kwa kukosa utaratibu  unaofaa  kwa kufuata sheria'' Gachagua alisema.

Gachagua alisema hayo siku moja tu baada ya kuvamiwa na makundi ya vijana waliokuwa wamejihami waliomvamia alipokuwa akihudhuria ibaada katika kanisa la PCEA Mwiki Kasarani siku ya jumapili ya tarehe 6  Aprili, 2025.

Hata hivyo hiyo inajiri siku moja baada ya Rais Ruto kukamilisha ziara yake ya siku tano eneo pana  la Mlima Kenya  na  hivyo basi kujihakikishia uuungwaji mkono kutoka kwa wakaazi wa  Mlima baada ya kuzindua na   kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Bwana Rigathi Gachagua mwanzoni mwa mwaka huu alikuwa ametoa taarifa kuwa  kabla ifike mwezi wa tano atakuwa ametoa msimamo wa kuzindua chama  na vilevile kuwahakikishia kuwa anawapa mwelekeo na msimamo wa wakazi wa  eneo lake la  Mlima Kenya Jinsi alivyoahidi 

Usiku  wa leo Gachagua atakuwa katika Runinga  ya KTN ambapo anatarajiwa  kutoa  taarifa ya msimamo wake kwa taifa na jinsi alivyojipanga  kisiasa.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved