logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maeneo ya Kenya ambako stima zitapotea leo, Jumatano - KPLC

KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Aprili 10, 2025.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri10 April 2025 - 08:00

Muhtasari


  • Kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti saba za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.
  • Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Murang'a, Nairobi, Kiambu, Kirinyaga, Kisii, Siaya, na Kakamega.

KPLC

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Aprili 10, 2025.

Katika taarifa ya siku ya Jumatano jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti saba za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Murang'a, Nairobi, Kiambu, Kirinyaga, Kisii, Siaya, na Kakamega. 

Katika kaunti ya Murang'a, maeneo ya Githingiri, Kandara Industrial Park , Rwathe, Gacharage, Muruka, Naaro, Ngararia, Kirwara, na Gatunyu yataathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Mwiki, na Karen katika kaunti ya Nairobi zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Ndekei, Old Kiambu, na Ndumberi katika kaunti ya Kiambu zitaathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Kirinyaga, maeneo ya Kiamaina, Gathuthuma, na Kagumo Sec School yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Eberege Tea Factory, Kenyoro, na Nyabitunwa katika kaunti ya Kisii zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Soko ya Uranga katika kaunti ya Siaya itakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Soko ya Harambee katika kaunti ya Kakamega pia itaathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved