
Watu saba walipoteza maisha yao mapema siku ya Ijumaa baada ya matatu ya abiria 14 kupoteza mwelekeo katika eneo la Kamandura kwenye barabara kuu ya Nairobi-Nakuru.
Gari lilitumbukia kwenye mteremko mkali na kubingiria mara kadhaa.
OCPD wa Limuru Mary Gachie alithibitisha kisa hicho na kusema kuwa matatu hiyo ambayo inamilikiwa na Kijabeline Sacco ilikuwa ikisafiri kutoka Nairobi kuelekea Kijabe.
Abiria watano walifariki papo hapo, huku wengine wawili wakifariki dunia wakati wakipokea matibabu. Watu wanne walionusurika, wote wakiwa katika hali mbaya, kwa sasa wanapokea matibabu katika Hospitali ya Tigoni.
Ajali
hiyo ilitokea mwendo wa saa mbili asubuhi, takriban kilomita moja kutoka eneo
la ajali nyingine mbaya iliyotokea Alhamisi jioni.