logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ibrahim Traore ajibu matamshi ya Amerika kuhusu vitisho vyao dhidi yake

Traore alijibu tetesi na Vitisho kutoka Marekani vya kumtaka asidhulumu raia kwa manufaa yake binafsi .

image
na Evans Omoto

Yanayojiri23 April 2025 - 09:10

Muhtasari


  • Traore katika  taarifa yake alieleza akisema kuwa wao kama taifa la Burkina Faso wana jukumu na wajibu wa kuhakikisha kuwa wanalinda maslahi ya taifa lao  ipasavyo.
  • Aliweza kusema kuwa kulingana na mambo yalivyokuwa wananchi walikuwa na chaguo mbili kuamua mustakabali wa maisha  yao ya mbeleni.

 Ibrahim Traore Rais wa Burkina Faso

Rais wa Burkina Faso Ibrahim Traore alijibu tetesi na Vitisho kutoka Marekani vya kumtaka asidhulumu raia kwa manufaa yake binafsi .

Traore katika  taarifa yake alieleza akisema kuwa wao kama taifa la Burkina Faso wana jukumu na wajibu wa kuhakikisha kuwa wanalinda maslahi ya taifa lao  ipasavyo.

Traore kulingana na mujibu wa maelezo yake aliwashujahisha wananchi kwa kuwaelezea kuwa afua zilikuwa ni mbili za  kujinasua  kutoka kwenye hali ambayo walikuwa ndani yake.

Aliweza kusema kuwa kulingana na mambo yalivyokuwa wananchi walikuwa na chaguo mbili kuamua mustakabali wa maisha  yao ya mbeleni.

Aliweza kusema kuwa wananchi walikuwa na jukumu la kupigania haki na uhuru wa  taifa  lao au wasalie  watumwa milele alisema kuwa kuna watu  ambao ni watumwa wa akili ili  kuweza kuwahudumia wakuu wao.

Alisema kuwa kuna watu ambao  wanahitalifiana na uhuru na uzalendo wa taifa la Burkina Faso ambapo huchukua ari ya moyo na uzalendo kuweza kupigania taifa lao.

''Kuna baadhi ya watu ambao  wanatupiga  vita  na kuhakikisha kuwa taifa letu linasambaratika lakini  tunawahakikishia kuwa tutapigania haki zetu  hadi tamati.

 Kuna  haya mashirika  ambayo  huitwa NGO ambayo huendeleza injili  ya  kusema kuwa  yanasaidia  watu hayo mashirika  ndio yaliyoangamiza  taifa la Libya.

Gaddafi yuko wapi walimwangamiza kwa  sababu waliona alikuwa  amepevuka  akili na kuwa kiongozi ambaye  alikuwa na maono mapevu kuweza kuhakikisha kuwa wananchi wa taifa  lake  wanaishi vizuri, haohao wazuri walimwangamiza.

Kwa hivyo kumekuwepo na vita duniani hasahasa vita vya pili vya  dunia ambapo mataifa mengi  duniani yaliweza kupigania uhuru wake na kuwa katika uongozi uliohuru. 

Taifa hili  ambalo lilipiganiwa na mababu ambao hawakukuwa wazawa wa taifa  hilo kwa sasa  baada ya kupevuka wanaanza  kutoa muongozo kwa mataifa mengine  kwa kutoa  vitisho.

Kama taifa tusimame imara na tuhakikishe kuwa tunalinda  taifa letu dhidi ya maadui ambao wanania  ya  kuja kutupora   raslimali zetu na kutuacha tukiwa masikini wa kutupwa.

 Ni lazima tusimame imara na  tuhakikishe  kuwa hatutingiziki kwa vyovyote vile  hio ndio itakuwa nguzo  na malengo ya  taifa letu'' Traore alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved