logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makundi ya haki za binadamu yalaumu serikali kwa kukosa kuwajibikia vifo vya raia

Cornelius Oduor Naibu mkurugenzi mkuu katika shirika la kutetea haki za binadamu la KHRC alisema serikali ilifeli pakubwa

image
na Evans Omoto

Yanayojiri23 April 2025 - 08:08

Muhtasari


  • Cornelius alikuwa akihojiwa  na runinga ya Citizen kuhusu hali ya utendakazi wa serikali pamoja na ushirikiano na makundi pamoja na mashirika ya kutetea haki za  binadamu.
  • Alifafanua akisema kuwa lilikuwa ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa lalama na kesi zote ambazo zishawahi ripotiwa kuhusu  mauaji ya kutatanisha na ambazo zilihusisha raia na maafisa  wa usalama ziwe zimeshughulikiwa kufikia sasa.

Coronelius Oduor Naibu mkurugenzi shirika la kutetea haki za binadamu KNHC

Cornelius Oduor  Naibu mkurugenzi mkuu katika shirika la kutetea haki za binadamu la KHRC alisema kuwa serikali ina rekodi mbovu ya utendakazi .

Cornelius alikuwa akihojiwa  na runinga ya Citizen kuhusu hali ya utendakazi wa serikali pamoja na ushirikiano na makundi pamoja na mashirika ya kutetea haki za  binadamu.

 Kulingana na mujibu wa maelezo yake Oduor aliweza kudunisha utendakazi wa serikali katika kushughulikia maswala ya  haki za binadamu kwa kuipa serikali kiwango cha chini cha rekodi ya utendakazi. 

Alifafanua akisema kuwa lilikuwa ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa lalama na kesi zote ambazo zishawahi ripotiwa kuhusu  mauaji ya kutatanisha na ambazo zilihusisha raia na maafisa  wa usalama ziwe zimeshughulikiwa kufikia sasa.

 Kulingana na maelezo ya Oduor  alisema kuwa haki  ilikosekana kwa wananchi wengi kutokanna na serikali kutokuwa na azma ya kuwahakikishia haki wale  wote  waliopoteza wapendwa wao.

Alisema kuwa matukio ya maandanamo yaliyofanyika mwaka wa 2024 Juni 26 yaliyosababisha vijana wengi wa kizazi cha Gen Z kuweza kupoteza maisha yalikuwwa ni matukio ya kusikitisha na  ambayo kwa mtazamo wake kufikia sasa haki ingekuwa imepatikana  pamoja na wahusika  kuwajibishwa ipasavyo.

''Ukiniuliza  mbona polisi kufikia sasa hawajawaajibisha na  kuwachukulia  hatua  za  kisheria wale wote waliohusika kinyume  cha  kisheria kwa kuwaangamiza vijana takribani  67 waliouawa wengine kwa mtutu wa  bunduki.

 Kufikia leo inasikitisha kuwa hamna jambo wala kesi yoyote  au hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya  wahuska hao hiyo ni  kuumanisha kuwa polisi hawafanyi kazi  kulingana na mujibu wa sheria na jinsi tunavyojua wanastahilikuwa wametekeleza wajibu wao ipasavyo.

Kufikia sasa ni mwaka mmoja hamna lolote lililojiri licha ya  rais  kutoa ahadi kuwa polisi watatengewa  bajeti yao na kutekeleza mambo yao bila kuingiliwa na  mtu  yeyote lakini tunachokishuhudia kwa  sasa  ni kinyume  cha hali ya juu  sana.

Swala la asasi huru kutekwa nyara na serikali ili zitekeleze  kazi  yake  kulingana na mapenzi ya serikali huo ni mkondo hatari kwa  taifa kile  ambacho kinastahili kuwa kinatekelezwa kufikia  sasa  ni kuwa familia za wale wote ambao walipoteza  wapenzi wao zinalilia haki kwa hivyo ningeomba serikali iwajibike ili tuweze  kujua  wote  waliotenda kinyume  na sheria waweze kukabiliwa na mkondo wa sheria'' Bwana Oduor  alieleza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved