logo

NOW ON AIR

Listen in Live

VIDEO: Mchezaji Wa Tanzania, Mrisho Khalfan, Afariki Baada Ya Kufunga Bao

VIDEO: Mchezaji Wa Tanzania, Mrisho Khalfan, Afariki Baada Ya Kufunga Bao

image
na

Michezo01 October 2020 - 16:23
ismail-mrisho
Kinda wa Mbao FC ya Mwanza, Ismail Mrisho Khalfan amefariki dunia leo baada ya kuzirai uwanjani alipogongana na beki wa Mwadui FC katika michuano ya Ligi ya Vijana wasiozidi umri wa miaka ishirini inayoendelea.
Kulingana na , mechi hiyo ilipigwa kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba na juhudi kubwa zilifanyika kuokoa maisha ya mchezaji huyo, bila mafanikio.
“Inaonekana alishafariki dunia pale uwanjani, tulifanya juhudi kubwa mimi na wenzangu. Tulisaidiana na watu wengine pia waliokuwa uwanjani, lakini ilionekana hakukuwa na majibu mazuri,” alisema mmoja wa madaktari waliojaribu kuokoa maisha ya kijana huyo.
Mwenyezi Mungu Amrehemu.
Tazama kanda ifuatayo...

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved