Asante kwa mafikira yake wengi utabasamu na kuachwa na kicheko vinyani mwao, kwa kweli Wakanai hajawahi hisi haya akizungumza na kutoa maoni yake.
Ushauri wake huwapa wanaume na wanawake lakini anafahamika kwa kuwaunga mkono wanawake na ushauri wake mwingi kuwapa wanawake.
Baadhi ya shauri ake ni kama vile zifuatazo;
1.Wanawake unapoenda kumtembelea mpenzi wako husikae kwenye kiti kama umeenda hospitalini kungoja muuguzi aseme uingie kuenda kumuona daktari
Enda kitandani kando yake fanya ulichokuwa umeenda kufanya.
2.Kama miguu yake haitetemeki unapomaliza kufanya kazi, ndugu yangu haujamaliza kazi rudi tena ukafanye kazi
3. Dadazanguni nenda shuleni ukatie bidii la sivyo fanya kazi kwa bidii ili huwe mtu maishani bali si kutegemea mfuko wa mwanamume.
Ndoa si kazi wala mwanaume si benki, husilete tu hips na vyeti vya kuzaliwa mezani.
4.Wanawake wengine husema kuwa aliyekuwa mpenzi wangu aliacha shimo kubwa katika moyo wangu...wacha kutudanganya tunajua aliacha shimo wapi.
5.Husimpende sana mwenzio kama pia naye hakupendi kwa maana upendo wa upande mmoja unaweza adhiri akili yako au usombwe na mawazo chungu nzima.
6. Mambo matatu ambayo hupaswi kumkejeli mwenzio nayo nikam vile watoto, pesa na ndoa, Mungu hupeana baraka zake kwa wakati wake
7.Hautawahi endelea na maisha ukiendelea kufanya ngono na aliyekuwwa mpenzi wako, kwa maana hisia zako hazitawahi hisha, ni muhimu kumuacha ex wako na ata sex uache.
Je unakubaliana na Wakanai, na ushauri upi ambao unauunga mkono?