logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru, wahudumu wa afya ndio mashujaa wa 2020- Infotrak

Katika utafiti wa kura ya maoni uliotolewa na kampuni ya  ,Infrotrak,  takriban nusu ya wakenya  wanasema serikali ilishughulikia  janga la corona kwa njia ya wastani .

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku25 January 2021 - 05:03

Muhtasari


  •  Katika utafiti wa kura ya maoni uliotolewa na kampuni ya  ,Infrotrak,  takriban nusu ya wakenya  wanasema serikali ilishughulikia  janga la corona kwa njia ya wastani .
  • Asilimia 11 ya wakenya walihisi  wizara ya afya ilikuwa ndio shujaa wao huku asilimia 10 wakimtaja naibu wa rais William Ruto kama shjaa wao .

 Wahudumu wa afya na rais Uhuru Kenyatta ndio mashujaa wa mwaka jana huku Polisi na bunge wakitajwa kama wakiorodheshwa katika nafasi za mwisho .

 Hii ni licha ya wakenya kuitwika lawama serikali ya Jubilee kutokana na jinsi ilivyoshughulikia uchumi wakati wa janga la Corona kwa kuondoa  afueni za ushuru ambazo zilikuwa zimetangazwa na serikali .

 Katika utafiti wa kura ya maoni uliotolewa na kampuni ya  ,Infrotrak,  takriban nusu ya wakenya  wanasema serikali ilishughulikia  janga la corona kwa njia ya wastani .

 

 Kulingana na matokeo ya kura hiyo yaliotangazwa siku ya jumapili  wahudumu wa afya wanashikilia uongozi kwa utendakazi wao  kwa asilimia 76 wakifuatwa na wanahabari kwa asilimia 72 huku mashirika ya kidini yakiwa katika nafasi ya tatu kwa asilimia 65  na rais Kenyatta ni wa nne kwa asimilia 63 .

 Utafiti huo  unaonyesha kwamba asilimia 42 ya wakenya wanahisi kwamba wahudumu wa afya  ndio waliokuwa mashujaa wa 2020 huku asilimia 12 w ya waliohojiwa  wakisema rasi uhuru ndiye shujaa wao .

Asilimia 11 ya wakenya walihisi  wizara ya afya ilikuwa ndio shujaa wao huku asilimia 10 wakimtaja naibu wa rais William Ruto kama shjaa wao .

 Na katika kitakachoikosesha usingizi serikali  takriban thuluthi mbili ya wakenya wanahisi kwamba kuondolewa kwa  afueni za ushuru sio hatua ambayo serikali ilizingatia athari zake kabla ya kuziondoa afueni hizo.

 Idadi kama hiyo inahisi kwamba serikali haikufanya vyema katika kusimamia  uchumi  huku asilimia 30 wakisema wameridhika na jinsi serikali ilivyoendesha uchumi wa taifa .

 Asilimia 45 hawakupendezwa na utendakazi wa polisi  wakifuatwa na bunge kwa asilimia 39 ,senate asilimia 35 na serikali z akaunti kwa asilimia 31.

 Utafiti huo ulifanywa kati ya disemba tarehe 27 na 29 mwaka jana  na uliwahusisha watu 800 walio na umri  wa zaidi ya miaka 18 katika kaunti 24 .

 

  

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved