logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila apuuzilia mbali 'Bottom up'

Bottom up, Raila apuuza mfumo wa kukuza uchumi

image
na Radio Jambo

Michezo12 August 2021 - 19:06

Muhtasari


• Raila alisema panafaa pawepo sera za kusaidia wawekezaji wa humu nchini ili kuimarisha biashara zao.

• Alisema mfumo huu wa kutoza kodi unahujumu sana wafanyibiashara wadogo wadogo.

Kiongozi wa ODM Raila Odinga

Aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga amekashifu mfumo wa uchumi wa ‘bottom up’ unaopendekezwa na naibu rais  William Ruto akisema kwamba mfumo huo ni wa  Kuwafumba wakenya macho.

Akizungumza katika eneo la Tigoni kaunti ya Kiambu siku ya Alhamisi alipokutana na wafanyibiashara Raila alisema kwamba njia mwafaka ya kuimarisha uchumi wa taifa ni kuimarisha uwekezaji wa humu nchini.

Kinara wa ODM alisema kwamba kama taifa haiwezekani kuimarisha uchumi wa taifa la Kenya kwa kuleta nchini wawekezaji wa kimataifa ambao lengo lao kuu ni kupata faida na kisha kurejesha pesa zao kwa wenye hisa wa kampuni zao.

Raila alisema panafaa pawepo sera za kusaidia wawekezaji wa humu nchini ili kuimarisha biashara zao.

Waziri mkuu wa zamani alikosoa sera ya utoaji kodi nchini akisema kwamba inawagandamiza wawekezaji wa humu nchini hatua ambayo imepelekea kusambaratika kwa biashara nyingi nchini.

Alisema mfumo huu wa kutoza kodi unahujumu sana wafanyibiashara wadogo wadogo.

“Lazima kuwe na mpango madhubuti, uliofikiriwa vizuri wa kujenga uchumi. Nchi yetu haitaweza kutegemea ahadi zilizojengwa kwa mifano ya uchumi ambayo hajajaribiwa na ambayo nguzo zake ni utapeli. Mawazo haya ni takataka” Raila alisema.

Raila alikariri msimamo wake wa kudhibiti ushuru na kodi wanazotozwa wawekezaji akisema kwamba zimekuwa kizingiti kikubwa katika sekta ya uwekezaji.

Naibu rais Wiliam Ruto na wandani wake wamekuwa wakipigia debe mfumo wa kuboresha uchumi unaolenga kukuza uchumi wa taifa kuanzia kwa mtu wa chini ‘Bottom up’ mfumo ambao Raila na wandani wake wamesema hauwezi kutekelezwa bali ni wa kuwahadaa tu wakenya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved