logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Picha) Rais Kenyatta, Ruto na Raila waketi kwa jukwaa moja wakati wa maadhimisho ya Mashujaa Day

Rais Uhuru Kenyatta, naibu rais William Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga waliketi katika jukwaa moja wakati Kenya ilisherehekea maadhimisho ya 58 ya siku ya Mashujaa.

image
na Radio Jambo

Michezo20 October 2021 - 11:57

Muhtasari


•Rais Uhuru Kenyatta, naibu rais William Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga waliketi katika jukwaa moja wakati Kenya ilikuwa inasherehekea maadhimisho ya 58 ya siku ya Mashujaa.

Rais Kenyatta na naibu rais William Ruto wakisalimiana wakati wa maadhimisho ya siku ya Mashujaa

Kaunti ya Kirinyaga ilikaribisha vigogo watatu wakuu wa siasa nchini wakati wa maadhimisho ya siku ya Mashujaa yaliyofanyika katika uwanja wa Wang'uru siku ya Jumanne.

Rais Uhuru Kenyatta, naibu rais William Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga waliketi katika jukwaa moja wakati Kenya ilikuwa inasherehekea maadhimisho ya 58 ya siku ya Mashujaa.

Rais Kenyatta na Ruto wasalimiana

Ruto hawajaonana jicho kwa jicho na rais Kenyatta tangu tarehe 1 mwezi Juni wakati wa maadhimisho ya siku ya Madaraka yaliyofanyika kaunti ya Kisumu.

Hivi majuzi Ruto alisema kwamba alisaidia Uhuru na Raila kupata  uongozi ila wakaungana pamoja kumpinga.

Mnamo Agosti 23, Uhuru aliambia Ruto hadharani ajiuzuru kutoka serikalini iwapo hajaridhishwa na namna kazi imekuwa ikitekelezwa badala ya kumkosoa akiwa serikalini.

Rais Kenyatta na DP Ruto

Naibu rais aliwasili mida ya saa tano asubuhi na kushangiliwa sana na watu kabla ya kuenda kusalimia waheshimiwa wengine ikiwemo Raila Odinga, Musalia Mudavadi, Gideon Moi kati ya wengine.

Baadae alienda kumkaribisha rais wa Malawi Lazarus Chakwera ambaye alikuwa mgeni mkuu katika maadhimisho ya siku ya Mashujaa mwaka huu.

Rais aliwasili baadae mida ya saa tano unusu na akazungushwa uwanjani huku akisalimia watu waliokuwa wamejumuika kabla ya kukaguwa gwaride la heshima lililojumuisha wanajeshi wa KDF.

Raila Odinga asalimia Gideon Moi na Moses Wetangula

Viongozi wengine ambao walihudhuria hafla hiyo ni pamoja na kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi, Kiongozi wa KANU Gideon Moi, Kiongozi wa Narc-Kenya Martha Karua na Jaji Mkuu Martha Koome.

Wengine ni pamoja na wabunge kutoka kaunti ya Kirinyaga, maseneta mbalimbali, spika wa bunge la kitaifa Justin Muturi na wa seneti Kenneth Lusaka, waziri Najib Balala, Farida Karoney na Fred Matiang'i.

Rais Kenyatta akikagua gwaride la heshima

Magavana ambao walihudhuria ni pamoja na Ann Waiguru wa Kirinyaga, Hassan Joho wa Mombasa, Mwangi wa Iria wa Murang'a, Martin Wambora wa Embu, Mutahi Kahiga wa Nyeri, Nderitu Muriithi wa Laikipia na Anyang' Nyong'o wa Kisumu.

(Utafsiri: Samuel Maina) 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved