logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwalimu Mkuu taabani kwa kupachika mwanafunzi mimba na kumpeleka kuiavya Kitui

Mwalimu mkuu alimpeleka mhasiriwa katika hospitali ndogo ya kibinafi ambako alipewa vidonge.

image
na Radio Jambo

Michezo22 February 2022 - 03:05

Muhtasari


•Mwanafunzi huyo wa darasa la nane anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Kitui baada ya kujifungua kijusi cha kiume cha miezi 5 kisicho hai 

•Baada ya kumeza vidonge hivyo mhasiriwa alianza kuumwa na tumbo  na kulazimu apelekwe hospitali.

Pregnant Student

Msichana mmoja wa miaka 16 aliponea kifo chupuchupu baada ya jaribio la kuavya mimba kuenda vibaya wikendi iliyopita.

Mwanafunzi huyo wa darasa la nane anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Kitui baada ya kujifungua kijusi cha kiume cha miezi 5 kisicho hai katika kituo cha afya cha Mumoni ambako alikimbizwa kufuatia maumivu.

Kulingana na kitengo cha DCI, mama ya mhasiriwa alisema bintiye alianza kulalamika kuhusu maumivu ya tumbo na ndiposa akamkimbiza hospitalini.

Baada ya kuhojiwa msichana huyo alifichua kuwa mwalimu mkuu wa shule yao, ambaye ndiye mwenye kumpachika ujauzito alimpeleka katika hospitali ndogo ya kibinafi katika maeneo ya Ishiara siku ya Jumamosi ambapo alipatiwa vidonge na kuagizwa ameze.

Baadae baada ya kumeza vidonge hivyo mhasiriwa alianza kuumwa na tumbo  na kulazimu apelekwe hospitali.

Shughuli ya kumsaka mshukiwa ambaye kwa sasa ameingia mitini pamoja na mmiliki wa hospitali iliyotekeleza mimba  imeanzishwa.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved