logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chochote nisemacho huwa kweli!- Arrow Bwoy aapa kutotumia kiki

Arrow Bwoy ameeleza wazi kuwa hatatumia kiki kupeleka mbele muziki wake

image
na

Michezo03 March 2022 - 07:55

Muhtasari


•Mwanamuziki Arrow Bwoy ameeleza wazi kuwa hatatumia kiki kupeleka mbele muziki wake ambao unaendelea kuimalika kila uchao.

 

Arrow Bwoy

Mwanamuziki Arrow Bwoy ametangaza wazi kuwa hatawahi kutumia kiki kupeleka mbele muziki wake ambao unaendelea kuimalika kila uchao.

Amesema kuwa chochote asemacho kwenye mitandao ya kijamii na katika mahojiano huwa cha kweli na sio kiki.

Mpenzi huyo wa Nadia Mukami ameapa kutotumia njia za mkato kukuza muziki wake kama wafanyavyo wasanii wengine wa hapa nchini

"Kwa wale wanaofanya kiki labda inawafanyia kazi .lakini kama Arrow Bwoy, watu watashabikia muziki wangu  hata bila kiki yoyote, Kiki haijawai kunifanyia kazi. Ukiona kitu au nikiposti kitu,fahamu ni kweli . nitakuwa nikifanya hivyo kutoka ndani ya moyo wangu," Alisema Arrow Bwoy.

 Hivi majuzi, mwimbaji huyo alitembelea mitaa ya mabanda ambapo aliwanunulia chakula mashabiki wake. Alidai kuwa hana uhakika kuhusu kiasi cha fedha ambacho alitumia siku hiyo. 

Arrow Bwoy aliwashukuru mashabiki wake huku akieleza kuwa wamekuwa wakimuunga mkono tangu alipojitosa kwenye tasnia ya muziki.

 "Nilifurahia sana kujumuika na mashabiki, nilirudi nyumbani nikiwa na hisia mingi, kwa Pesa nilizotumia kununua. Niliweka tabasamu kwa watu. nyuso na siwezi kuweka bei kusaidia." 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved