Pesa ni kiungo muhimu sana katika maisha ya mwanadamu yeyote. Tunahitaji fedha ili kufanikiwa kukidhi mahitaji ya kimsingi na tuweze kuishi maisha ya starehe.
Kila siku Wakenya tunapambana kusaka pesa na kila tunapopata kidogo mahitaji yetu yanatusukuma kutafuta zaidi.Wakati watu wanataka kutengeneza pesa zaidi, wengi hupatwa na wazo la kuwekeza.
Hata hivyo, jinsi ya kuwekeza pesa kwa busara imebaki kuwa kitendawili kwa wengi.Huenda wewe ni miongoni mwa kundi la Wakenya ambao wameshindwa kabisa kupata njia ya uhakika na rahisi ya kuwekeza pesa zako?
Usijali tena. Adam MMF inakuletea njia ya uhakika ya kuwekeza pesa zako bila kusumbuka sana. Adam MMF inakuhakikishia usalama wa pesa zako na mapato ya kihakika bila wewe kuweka juhudi nyingi.
Pesa Smart na Adam MMF ni njia mpya rahisi ya uwekezaji kwani unahitajika tu kuweka pesa zako kisha kuendelea na shughuli zako za kawaida huku kiasi ulichoweka kikiendelea kukua zaidi.
Adam MMF ni shirika lisilo la kiserikali ambalo hukusanya pesa kutoka kwa watu mbalimbali na kuziwekeza kwa busara katika masoko makubwa ya fedha kisha kugawana faida na waliowekeza.
Baada ya kuwekeza na Adam MMF unatakiwa kutulia tu na kuacha pesa zako zikufanyie kazi. Mwisho wa yote umehakikishiwa kurudi salama kwa fedha zako pamoja na faida ya kusisimua.
1. Fahamu jinsi ya kuwekeza pesa na Adam MMF:-Kujiunga na kundi kubwa la Wakenya ambao tayari wananufaika kutokana na Pesa Smart ni rahisi sana. Chukua simu yako ya mkono ubofye nambari *227# ili kuwezesha huduma ya Adam MMF au udownload Mpesa App na ugundue Adam App kisha weka kodi A100, A105 au A975 huku ukijisajili kuwezesha Pesa Smart.
Baada ya kujisajili na Adam MMF unaweza kuweka kuanzia kiwango cha Ksh100 ili kuanza kufurahia faida bila jasho.
2. Manufaa ya kutumia Adam MMF:
i )Kwa mwaka mmoja unaweza kupata faida ya hadi asilimia 10% ya kiasi ulichowekeza.
ii) Unaweza kuwekeza kiasi kidogo zaidi hadi Kshs 100.
iii) Unaweza kutoa kiasi uwekezaji wako ndani ya masaa 48.
iv) Unaweza kuangalia salio lako wakati wowote.
v) Unaweza kujiandikisha kwa mpangilio ulio kwenye Master card au Visa yako.
vi) Unaweza kuweka akiba rahisi kutoka kwa Mpesa au Mastercard & Visa.
vii) Fedha zako huwekezwa katika Masoko ya Pesa ambayo yanadhibitiwa na CMA.
viii) Unaweza kupata mikopo zaidi ya kiasi ulichowekeza kutoka kwa washirika wetu wowote wa kifedha.
Ix) Unaweza kuwekeza kupitia USSD. Katika Adam MMF unapata pesa zaidi bila kufanya kazi zaidi. Mradi umeweka kiasi fulani cha pesa, unahakikishia faida ya kusisimua kutokana na fedha ulizowekeza.
