logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chagua Rais aliye na heshima,' Martha Karua awahimiza Wakenya

Karua alipigia debe mgombea urais wa Azimio La Umoja Raila Odinga,

image
na Radio Jambo

Football10 June 2022 - 13:39

Muhtasari


  • Alisisitiza kwamba kiongozi ambaye haonyeshi heshima kwa wale wanaofanya nao kazi hawezi kuheshimu raia wa kawaida

 Mgombea mwenza wa urais  Azimio La Umoja Martha Karua mnamo Ijumaa aliongoza kampeni za muungano huo katika kaunti za eneo la Mashariki za Makueni na Kitui.

Karua alipigia debe mgombea urais wa Azimio La Umoja Raila Odinga, akiwataka Wakenya kuwapigia kura wagombeaji chini ya mwavuli wa Azimio katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Agosti.

Alisisitiza kwamba kiongozi ambaye haonyeshi heshima kwa wale wanaofanya nao kazi hawezi kuheshimu raia wa kawaida.

“Kama huna heshima kwa wenzako, pia hutawaheshimu wananchi, ukitaka urais, mheshimu rais aliye madarakani... Na haimaanishi kwamba usimkosee bali fanya kwa utaratibu. hiyo ni ya utaratibu na ina msingi,” alisema Karua, ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha NARC-Kenya.

Aliongeza:

"Ukichagua viongozi bila heshima, utakuwa umejidhulumu mwenyewe na pia utadharauliwa. Kibaki alikuwa mnyenyekevu lakini uliona matunda ya uongozi wake. "

Kiongozi huyo wa NARC-Kenya alisema kitu pekee ambacho nchi hiyo inahitaji kwa sasa ili kusonga mbele ni uongozi bora, ambao alisema utatolewa na Odinga na yeye mwenyewe.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved