logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wekeni bando tayari! Diamond na Nameless watangaza jambo lao kubwa Julai 14

Nameless watakuwa wanakutana kwenye jukwaa na Diamond kwa mara ya kwanza.

image
na Radio Jambo

Burudani16 June 2023 - 07:59

Muhtasari


โ€ข Nameless ni mmoja wa wasanii wachache ambao walianza muziki wa Zaidi ya miongo miwili iliyopita na ambao hadi sasa bado wanazidi kutamba.

Diamond na Nameless watangaza jambo lao kubwa Julai 14.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya muziki wa Kenya na Tanzania, wasanii Nameless na Diamond wanatarajiwa kukutana kwenye tamasha ambalo litafanyika mwezi Julai nchini Uganda.

Tamasha hio ambalo limetangazwa kufanyika tarehe 14 Julai katika ukumbi maarufu wa Kololo litakuwa la kwanza kabisa kwa wababe hao wawili kukutana kwenye ukumbi mmoja.

Diamond kutoka Tanzania na Nameless kutoka Kenya ndio watakuwa wasanii wakubwa kutumbuiza kwenye tamasha hilo ambalo litakuwa linawajumuisha pia makumi ya wasanii wa Uganda.

Tamasha hilo litakuwa linaongozwa na mchekeshaji maarufu kutoka Uganda, Alex Muhangi na miongoni mwa wasanii wa Uganda ambao watapata nafasi adimu ya kutumbuiza na miamba hao wawili ni pamoja na King Saha, Spice Diana, Winnie Nwagi, Karole Kasita miongoni mwa wengine.

Nameless ni mmoja wa wasanii wachache ambao walianza muziki wa Zaidi ya miongo miwili iliyopita na ambao hadi sasa bado wanazidi kutamba na kupalilia jina lao katika tasnia ya Sanaa.

Vile vile, Diamond ni mmoja wa waanzilishi wa Sanaa ya kizazi kipya maarufu Bongo Flava nchini Tanzania na ambaye anakaribia miaka 15 kwenye gemu la Bongo.

Ikumbukwe siku mbili zilizopita, jukwaa la utiririshaji muziki la Boomplay lilimtangaza Diamond kuwa msanii wa kwanza kabisa kuwahi kutokea, ambaye amepiga namba na takwimu za juu Zaidi kwenye kukwaa hilo, kutoka ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa Boomplay, Diamond almaarufu Simba ndiye msanii wa kwanza kupiga namba Zaidi ya milioni 300 kwenye takwimu za utiririshaji.

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoยฉ Radio Jambo 2026. All rights reserved