logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Siondoki sokoni mimi mwenyewe ndio soko, nilisonga kando kidogo na nimerudi - Akothee

Mimi niko na majukumu mengi ya kutekeleza. Huwa sifanyi maamuzi kwa kuzingatia njaa - Akothee.

image
na Radio Jambo

Michezo01 November 2023 - 06:25

Muhtasari


• Pia alikanusha madai kwamba Omosh ni kijana kutoka Pakistan, akisema kwamba ni wa Uswizi na hata walikutana huko na mamake pia.

• "Na nimerudi vile mnaona mimi bado wa moto. siwezi ondoka sokoni, nilisonga tu kando kidogo. soko ni hapo hapo tunaoga na tunakaukia hapo," alisisitiza.

wakifurahia fungate jijini Santorini, Ugiriki.

Licha ya kuwa na umri wa miaka Zaidi ya 40, msanii na mjasiriamali Akothee amesisitiza kwamba hayuko tayari kuachana na suala la kutafuta mapenzi.

Akothee amesema haya licha ya kwamba pia hajakuwa na bahati ya kupata mwanamume wa kudumu naye kwa muda mrefu, wa hivi karibuni akiwa mpenzi wake kutoka Uswizi ambaye alivunja ndoa yao miezi 5 tu baada ya harusi ya kifahari.

Akothee anasisitiza kwamba hataondoka sokoni muda wowote kwani yeye mwenyewe ndiye soko na atazidi kusukuma hadi pale nyota yake itakaposimama.

“Kama nilivyowaambia awali, ukishafikisha miaka 40, baadhi yenu ni wadogo kiumri, unatashangaa jinsi Akothee anavyosahau kuvunjwa moyo haraka hivyo. Mimi niko na majukumu mengi ya kutekeleza. Huwa sifanyi maamuzi kwa kuzingatia njaa, maamuzi yangu yanazingatia hisia wakati huo,” alisema.

“Mimi nilikuwa nimezama kwenye mapenzi kusema ukweli, na nilikuwa nimepata pacha wangu, mbona nisifunge ndoa na yeye? Kama haitakwenda jinsi nilivyotarajia tena tunarudi, kama ambavyo niliwaambia mimi siondoki sokoni, mimi ndio soko mwenyewe. Mbona niondoke soko langu, tunakanyagana tu hapo,” Akothee aliongeza.

"Na nimerudi vile mnaona mimi bado wa moto. siwezi ondoka sokoni, nilisonga tu kando kidogo. soko ni hapo hapo tunaoga na tunakaukia hapo," alisisitiza.

Pia alikanusha madai kwamba Omosh ni kijana kutoka Pakistan, akisema kwamba ni wa Uswizi na hata walikutana huko na mamake pia.

“Omosh ni Mswizi anatoka katika familia iliyochanganyika. Mamake ni singo ana watoto 5, yeye ni mzawa wa pili. Nilikutana na mamake wakati tulienda Italia, alifurahia kunijua niliongea na yeye kwa Kijerumani na nilimwambia kwamba mimi ni mama wa watoto 5 na nimekuwa katika mahusiano mengi yaliyofeli kwa hiyo jua mvulana wako ndio anafuata,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved