logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Neymah Jr arejea uwanjani baada ya kupata jeraha lililomweka nje kwa zaidi ya mwaka 1

Aliingia katika dakika ya 77 kwenye mechi kati ya Al Hilal na Al-Ain kwenye ligi ya mabingwa barani Asia

image
na Brandon Asiema

Michezo22 October 2024 - 08:50

Muhtasari


  • Alipata jeraha lililomweka nje kwa zaidi ya mwaka mmoja akichezea timu ya taifa dhidi ya Uruguay Oktoba mwaka wa 2023

Mshambuliaji wa timu ya Al Hilal inayoshiriki Saudi Pro League Neymar Jr, amerejea kucheza soka baada ya kupata jeraha la goti lililomweka nje kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Neymah alirejea kusakata kabumbu katika mechi kati ya Al Hilal na Al-Ain iliyokamilika kwa ushindi wa Al-Hilal wa mabao 5 kwa 4 kwenye ligi ya klabu bingwa barani Asia.

Mchezaji huyo raia wa Brazil aliingia mchezoni akichukua nafasi ya Nasser Al-Dawsari aliyepata jeraha katika dakika ya 77 ya mchezo.

Jeraha la Neymah limemweka nje kwa takribani siku 369. Neymah alipata jeraha hilo akichezea timu ya taifa katika mechi ya kufuzu kombe la dunia la mwaka 2026dhidi ya Uruguay mnamo October 17, mwaka wa 2023.

“Nahisi vizuri, ni ngumu lakini. Siku zote nina timu nzuri lakini nina furaha sana nimerudi.” Alisema Neymah baada ya kucheza mechi aliyoingizwa kipindi cha pili.

Wakati wa kupata jeraha, mchezaji huyo alikuwa amejiunga na Al Hilal miezi 2 tu akitokea Paris Saint Germain kwa kitika cha Yuro milioni 90.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved