logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanachama wapya katika bodi ya usimamizi wa Sports Kenya wazinduliwa rasmi na waziri Murkomen

Wanachama hao walizuru miradi inayoendelezwa ya Sports Kenya ya ukarabati wa viwanja jijini Nairobi

image
na Brandon Asiema

Michezo28 November 2024 - 16:02

Muhtasari


  • Wanachama hao wapya walifanya ziara ya kufahamu miradi ya shirika la Sports Kenya katika jiji la Nairobi wakiwa pamoja na waziri wa michezo Kipchumba  Murkomen.
  • uzinduliwa kwa bodi hiyo kunajiri wakati Kenya inajiandaa kuwa mwenyeji wa mashindano ya CHAN yatakayoandaliwa klwa ushirikiano na mataifa ya Tanzania na Uganda. 


Waziri wa michezo, sanaa na maswala ya vijana Kipchumba Murkomen, mnamo Alhamisi asubuhi amezindua bodi mpya ya Sports Kenya.

Sports Kenya na ni shirika la serikali ambalo linasimamia vifaa vya michezo ikiwemo viwanja, kuendesha programu za michezo  pamoja na kukuza utalii wa michezo nchini.

Kuzinduliwa kwa bodi hiyo kunajiri wakati Kenya inajiandaa kuwa mwenyeji wa mashindano ya CHAN yatakayoandaliwa klwa ushirikiano na mataifa ya Tanzania na Uganda. Vile vile, nchi hizo tatu za Afrika Mashariki zinatarajia kuandaa kipute cha AFCON cha mwaka 2027, ambapo Kenya ipo mbioni kukarabati viwanja vitakavyotumika katika michuano hiyo.

Bodi iliyoasisiwa inatarajiwa kuhakikisha viwanja hivyo vinakuwa tayari kuandaa CHAN ya mwakani. Waziri Murkomen amesema kuwa kupitia bodi hiyo, serikali lazima imalize ukarabati wa viwanja kwa muda unaostahili, kuimarisha ubora wa viwanja hivyo na kuhakikisha vinalindwa kupitia uongozi ulio bora.

Bodi hiyo inayoongozwa na mwenyekiti Mark Lomunokol, ina wanachama wageni ambao ni William Odaji, Mohamed Shoaib Vayani na Richard Kimutai Chemweno.

Wanachama hao wapya walifanya ziara ya kufahamu miradi ya shirika la Sports Kenya katika jiji la Nairobi. Wakiwa pamoja na waziri Murkomen Alhamisi, walizuru uwanja wa Kasarani na Nyayo unaofanyiwa ukarabati pamoja na uwanja mpya unaojengwa wa Talanta Sports City.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved