Wachezaji wa Gor Mahia washerehekea bao lao dhidi ya Mara Sugar
Gor Mahia walikwea hadi nafasi ya tano kwenye jedwali la Ligi Kuu ya Kenya baada ya kuandikisha ushindi wa 2-0 dhidi ya Mara Sugar katika uwanja wa Raila Odinga huko Homa Bay.
Austin Odhiambo na Gideon Bandeka walitia kimyani mabao yaliyohakikishia Gor Mahia ushindi.
Ushindi huo ulitamatisha msururu wa matokeo duni K’Ogalo walikuwa wameandikisha msimu huu kabla ya mechi hiyo.
Kocha Leonardo Neiva, raia wa Brazil, alijipata mashakani alipotimuliwa baada ya mashabiki kumwelekezea gadhabu kutokana na utendakazi usioridhisha.
Wasimamizi wa klabu waliteua mchezaji wa zamani Zedekiah ‘Zico’ Otieno kuchukua hatamu za uongozi huku wakiimarisha kampeni yard kutafuta kocha mpya.
Jumamosi, aliyekuwa Waziri Mkuu na mlezi wa Gor Mahia Raila Odinga alikuwa miongoni mwa mashabiki walioshuhudia ushindi huo muhimu wa K'Ogalo.