logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Athari za kumchapa na kumdhalilisha mtoto wako, Sheila Akwara asimulia

Athari za kumchapa na kumdhalilisha mtoto wako, Sheila Akwara asimulia

image
na

Football02 October 2020 - 10:19
Screenshot_from_2019_11_25_17_18_18__1574692793_46982
Je, hivi unaamini kumchapa mtoto wako kunaweza kusababisha maumivu ya kisaikolojia?

Sheilla Akwara ni mojawapo ya watoto waliopitia katika mazingira haya ya maonevu.

Mwanadada huyu aliihama nchi yake na kuzamia Marekani ili kupata masomo zaidi.

https://www.instagram.com/p/B5SP-2ogXJ1/

Akisimulia Bustani la Massawe maisha yake, Sheila amesema kuwa alichukizwa na jinsi shuleni alikuwa anapata kichapo cha mbwa.

"Shuleni tulipigwa na walimu kinyama. Shule hiyo nilihamia baada ya kutofanya vizuri katika shule niliyosomea..." Sheila akisimulia Massawe.

https://www.instagram.com/p/B5ShG0bAMu8/

Kuchapwa kila mara kulimuumiza kisaikolojia na kuona thamani yake haipo na hivyo akaamua kujitoa uhai.

Hakuweza kuangamia kwani alipata usaidizi wa dharura na kukwepa mauti.

Kwa sasa Sheila anafanya juhudi za kuhamasisha jamii kuhusu kuwapiga na kuwadhalimu watoto wadogo.

Sheila anawahamasisha watu kuhusu maisha na kutoa msisitizo kwa wazazi kuwasikiliza wanao kwa kiwango kikubwa badala ya kuwaadhibu.

Mwanadada huyu hakupenda mazingira ya pale nyumbani kwao,

"Uncle walikuwa wakija kwetu na kusema kuwa mama amezaa wasichana ambao hawawezi kumsaidia. Walitaka awe na wavulana." Alisema Sheila.

Aidha presha za wazazi awe mhandisi au daktari zilimnyima uhuru wa kuchagua anachotaka maishani.

"Wazazi wanataka ukue mhandisi au daktari..." Sheila alizidi kusema.

Kuhusu nia na azma ya kutoka Marekani, mwanadada huyu amesema kuwa hakufurahishwa na vitendo ya wanarika kujiua.

"Nilikuona nikiona story hizi kwa social media watu walijiua kwa sababu ya depression. Nilirudi kuhamasisha watu. Kwa nini watu wajiue? Ni presha nyingi ya wazazi na jamii..." Alisema Sheila.

"Naambia watu wakuwe na vision. Nilipoenda Marekani maisha yalikuwa rahisi,nilidhani nitaishi na depression maisha yangu..." Sheila.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved