logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Umemwandalia meza machoni mwa watesi wake na kumpaka mafuta,'Kanze Dena ampongeza Kambua

Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram Kambua alitangaza habari njema

image
na Radio Jambo

Football16 October 2020 - 14:32

Muhtasari


  • Mungu amemwandalia meza mbele ya watesi wake Kanze Dena ampongeza Kambua
  • Kambua alitangaza habari njema kupitia ukurasa wake wa instagram

Msanii Kambua Manundu na mumewe Jackson Mathu wanatarajia mtoto wao wa pili, hii ni baada ya kubarikiwa na kifungua mimba wake mwaka jana na ambaye alifikisha mwaka mmoja Agosti mwaka huu.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram Kambua alitangaza habari njema  kuwa na ujauzito wa pili na kuandika ujumbe huu,

"Mungu wa Sarah na Mungu wa Hannah na mUngu wa Kambua punde tu nilipodhani kuwa umetenda ya kutosha umetenda tena." Aliandika Kambua.

 

Wasanii,wanahabari na mashabiki walimpongeza huku aliyekuwa mtangazaji wa runinga ya Citizen Kanze Dena akimpongeza na kusema kuwa Mungu amemwandalia Kambua meza mbele ya watesi wake.

Na huu hapa ujumbe wake Kanze Dena;

"Kila siku ....kila saa..Mungu umwaminifu...umemwandalia meza @kambuamuziki machoni mwa watesi wake na ukampaka mafuta..hakika wema nazo Fadhili zitamfuata dada na uzao wake siku zote za maisha yao.! JEHOVAH BABA MUNGU."Kanze Alinakili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved