logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi wa chuo kikuu auza figo yake ili kumnunulia mpenziwe Iphone 14

Simu ya Iphone 14 ilizinduliwa takribani mwezi mmoja uliopita na inauzwa kwa bei ya Ksh 299,000.

image
na Radio Jambo

Football17 October 2022 - 09:50

Muhtasari


• Iliarifiwa kwamba alimnunulia mpenzi wake simu ya gharama kwa sababu ya kiwango cha upendo wake kwake.

Mapenzi ni kipofu. Mapenzi yanaweza kusababisha mtu akatekeleza kwenye maamuzi magumu pasi na kujua wala kujali matokeo yake mbeleni.

Taarifa za mwanafunzi mmoja wa chuo kikuu aliyesemekana kuuza figo yake moja kwa ajili ya kumnunulia mpenzi wake simu mpya aina ya Iphone 14 pro max zimewashangaza sana wanamitandao.

Habari hizo zilizochapishwa kwenye vyombo vingi vya habari nchini Nigeria zilieleza kwamba kijana huyo mwanafunzi wa chuo kikuu cha Port Harcourt alipita mipaka katika kuonesha mapenzi yake kwa mpenzi wake kwa kuiweka rehani figo yake moja ili kumnunulia zawadi ya simu kali.

Iliarifiwa kwamba alimnunulia mpenzi wake simu ya gharama kwa sababu ya kiwango cha upendo wake kwake.

Picha zinazozunguka kwenye mitandao ya kijamii zinamuonyesha akiwa ameshika iPhone huku akionyesha tumbo lake na plasta upande wa kulia wa karibu na mahali figo inakusudiwa kuwa.

Mtumiaji wa mitandao ya kijamii alipakia hadithi hiyo, akiandika;

”Mwanafunzi wa Uniport ametoka kuuza FIGO Ili kumnunulia Mpenzi wake IPHONE 14. Anasema pia anampenda msichana huyo”

Wanamitandao walishangazwa na kitendo hicho amabcho wengi walikifananisha na kujitoa kafara huku wengine pia wakisema ni kama kujitoa mhanga kwa ajili ya mapenzi.

“Wasiwasi wangu ni kama anaweza kuutumia vyema UWEKEZAJI huu wa maisha. Je, anajua jinsi ya Kurudisha uwekezaji huu?” mmoja aliuliza.

Simu hiyo ya Iphone 14 ilizinduliwa takribani mwezi mmoja uliopita na kampuni ya Apple na kwa bei ya wastani nchini Kenya inauzwa kwa takribani laki 2 na elfu tisini na tisa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved