logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Madaktari wa Maradona washtakiwa kwa kifo chake

Washtakiwa wanasema Maradona alikataa matibabu zaidi na alipaswa kukaa hospitalini kwa muda mrefu baada ya upasuaji wake.

image
na BBC NEWS

Football12 March 2025 - 14:21

Muhtasari


  • Waendesha mashtaka wanadai kuwa kifo cha Maradona kingeweza kuepukwa na kuwashutumu wafanyakazi wa hospitali hiyo kwa uzembe wa kiafya.

Diego Maradona

Kesi iliyosubiriwa kwa muda mrefu ya wahudumu wa matibabu waliomtibu gwiji wa soka wa Argentina marehemu Diego Maradona imeanza katika mji mkuu, Buenos Aires.

Maradona alikuwa akiendelea kupata nafuu alipofariki kutokana na mshtuko wa moyo akiwa nyumbani kwake mwaka wa 2020, akiwa na umri wa miaka 60. Alikuwa akipata nafuu nyumbani baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuganda kwa damu kwenye ubongo mapema mwezi huo.

Waendesha mashtaka wanadai kuwa kifo cha Maradona kingeweza kuepukwa na kuwashutumu wafanyakazi wa hospitali hiyo kwa uzembe wa kiafya.

Washtakiwa wanasema Maradona alikataa matibabu zaidi na alipaswa kukaa hospitalini kwa muda mrefu baada ya upasuaji wake.

Wanakabiliwa na kifungo cha kati ya miaka minane na 25 ikiwa watapatikana na hatia kwa shtaka la "mauaji ya kukusudia".


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved