logo

NOW ON AIR

Listen in Live

William Saliba azungumzia madai yanayomuhusisha na kuhamia Real Madrid

Madrid haijamsajili beki wa kati tangu Antonio Rudiger alipowasili mwaka 2022 na hawajalipa pesa kwa muda mrefu zaidi.

image
na Japheth Nyongesa

Football12 March 2025 - 09:03

Muhtasari


  • Beki wa Arsenal William Saliba amepuuzilia mbali uvumi unaoendelea kuhusu uwezekano wa uhamisho wake wa baadaye kwenda Real Madrid.
  • Beki huyo ana mkataba na Arsenal hadi 2027 na anasisitiza kuwa hakuna "haraka" ya kuingia katika mazungumzo juu ya mkataba mpya wakati huu.

Beki wa Arsenal William Saliba amepuuzilia mbali uvumi unaoendelea kuhusu uwezekano wa uhamisho wake wa baadaye kwenda Real Madrid, klabu ambayo inahitaji sana kuimarisha safu ya kati.

Madrid haijamsajili beki wa kati tangu Antonio Rudiger alipowasili mwaka 2022 na hawajalipa pesa kwa muda mrefu zaidi.

Lakini baada ya  Nacho kuondoka msimu uliopita wa joto na kujeruhiwa kwa David Alaba na Eder Militao, kikosi hicho kimeachwa katika hali mbaya msimu huu. Aurelien Tchouameni ameingizwa kama mchezaji wa dharura, huku Raul Asencio na Jacobo Ramon pia wakiingia katika kikosi cha kwanza ili kuziba pengo.

Madrid wamekuwa wakihusishwa na kila aina ya chaguzi za kuajiri, kutoka kwa nyota Virgil van Dijk wa Livepool na  kwa upande mwingine William Saliba wa Arsenal ambaye ametajwa kama mchezaji anayekaribia kilele chake katikati soka

Hata hivyo, Mfaransa huyo ambaye alilazimika kuwa mvumilivu kwa nafasi yake ya Arsenal baada ya kuwasili kama kijana asiyejulikana na kutumia misimu kadhaa nje kwa mkopo, hashinikizi kuhama.

"Kwangu mimi, nina furaha sana hapa. Nimekuwa hapa kwa miaka miwili na nusu. Hakuna kitu. Nina furaha na ninataka kuendelea kuwa hapa."Saliba aliwaeleza wanahabari.

Beki huyo ana mkataba na Arsenal hadi 2027 na anasisitiza kuwa hakuna "haraka" ya kuingia katika mazungumzo juu ya mkataba mpya wakati huu. "Kuna miaka kadhaa iliyobaki]. Nina furaha hapa, hiyo ndiyo hali halisi."

Rudiger tayari amezungumzia sifa za Saliba, hivi karibuni alimujumuisha mchezaji huyo miongoni mwa mabeki watatu wa kati anaowaona kuwa bora zaidi.

"Saliba, Virgil van Dijk na... Nampenda Gabriel kutoka Arsenal, kwa kweli anasukuma," alisema Mjerumani huyo.

"Nafurahia tu, kwa mfano ukiona Arsenal, mabeki wawili wa kati wakicheza pamoja, wamekuwa wakifanya kazi nzuri kwa miaka miwili sasa.

"Mabadiliko kutoka Arsenal ambayo yalikuwa kabla kidogo hadi sasa, hayo mawili ni nguzo zake, Gabriel na Saliba. Gabriel ni kiongozi mwenye uzuri zaidi, na Saliba... Ndugu huyu anacheza kwa usafi. Unapaswa kutoa kwa ajili yake. Anaonekana kama kiongozi wa kimya kimya, na napenda hilo." alisema Rudigar


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved