logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kocha Mikel Arteta adokeza kuhusu kurejea kwa Kai Havertz

Arteta amesema ana matumaini Kai Havertz atarejea uwanjani mapema kuliko ilivyotarajiwa.

image
na Samuel Mainajournalist

Football19 April 2025 - 08:31

Muhtasari


  • Ingawa hawezi kurejea kwa muda wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya PSG, Arteta anaamini anaweza kuwa tayari iwapo Arsenal watafuzu hadi fainali.
  • “Anavyofanya kazi kila siku—yupo ukumbini akijifua, anawasukuma wote—sioni kama kuna kitu kinachoweza kumzuia tena.,” Arteta alisema.

Kai Havertz

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, amesema ana matumaini Kai Havertz atarejea uwanjani mapema kuliko ilivyotarajiwa, kufuatia maendeleo mazuri ya nyota huyo wa Ujerumani anayepambana kupona jeraha la msuli wa paja.

Havertz alitarajiwa kukosa msimu mzima baada ya kufanyiwa upasuaji mwezi Februari, alipoumia wakati wa kambi ya mazoezi ya hali ya joto mjini Dubai.

Ingawa hawezi kurejea kwa muda wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Paris Saint-Germain, Arteta anaamini kiungo huyo anaweza kuwa tayari iwapo Arsenal watafuzu hadi fainali itakayopigwa mjini Munich, Mei 31.

“Kwa nusu fainali? Nafikiri hiyo ni mapema sana,” Arteta alisema. “Lakini kama ningelazimika kubashiri iwapo atarudi mapema kuliko ilivyotarajiwa, ningesema: ‘Ndiyo’.

“Anavyofanya kazi kila siku—yupo ukumbini akijifua, anawasukuma wote—sioni kama kuna kitu kinachoweza kumzuia tena.”

Arsenal walifanikiwa kufuzu kwa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009, baada ya kuibuka na ushindi wa jumla wa mabao 5-1 dhidi ya Real Madrid, licha ya kutowajumuisha Havertz na Gabriel Jesus.

Ufanisi huo wa Ulaya umewafariji mashabiki huku matumaini yao ya ubingwa wa Ligi Kuu ya England yakizidi kufifia. Arsenal wako njiani kumaliza nafasi ya pili kwa msimu wa tatu mfululizo, wakiachwa pointi 13 nyuma ya vinara Liverpool huku zikiwa zimesalia mechi sita.

Liverpool wanaweza kutawazwa mabingwa mapema siku ya Jumapili iwapo watawashinda Leicester na Arsenal wapoteze dhidi ya Ipswich, walioko chini ya msimamo.

Arteta amewataka wachezaji wake wasilegeze kamba, akisema kuwa nafasi ya kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa msimu ujao bado haijathibitishwa.

“Tutasimama imara kuhakikisha tunashinda mechi na hilo halitokei,” alisema Mhispania huyo kuhusu uwezekano wa Liverpool kutwaa taji Jumapili. “Tunapaswa kuamka na kuanza kushinda mechi.”

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved