logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tunachinjwa kama kuku-Wakazi wa Sondu wazungumza kuhusu mapigano ya mpaka

Mnamo 1992, mpaka ulirudishwa hadi Kaunti ya Kericho

image
na

Uchaguzi04 October 2023 - 13:39

Muhtasari


  • Mapigano hayo yalitokea Jumanne usiku katika mpaka wa Kericho-Kisumu karibu na soko la Sondu.

Wakaazi wa Sondu kaunti ya Kisumu wanaitaka serikali kuingilia kati kufuatia mapigano yaliyosababisha vifo vya watatu Jumanne usiku.

Mapigano hayo yalitokea Jumanne usiku katika mpaka wa Kericho-Kisumu karibu na soko la Sondu.

Wakazi hao wakizungumza na vyombo vya habari siku ya Jumatano walisema wanapata riziki zao kutoka soko la Sondu na kwamba mapigano hayo yamewavuruga shughuli zao za kuwaingizia kipato.

"Mimi naishi Sondou na sisi wanawake, Sondu ndo mahali petu pa ukubwa. Na sahii hatuezi ukubwa, tunakufa njaa," mwanamke mmoja alisema.

Waliuliza viongozi wao wanafanya nini kuhusu mapigano hayo ambayo yalikuwa yanawadhuru na kuwaacha wengine wakiwa wamekufa.

"Na hawa viongozi kwa nini wasitusaidie? Wanatuua kama kuku, MCA uko wapi? Ojienda uko wapi? Nyong'o uko wapi? Tunaumia. Sisi wanawake sisi ndo tutaumia sababu sisi ndo tunatafuta vile watoto wanakula," mmoja wa wakazi alisema.

Baadhi ya waliojeruhiwa wakati wa makabiliano hayo wamelazwa katika hospitali kwa ajili ya matibabu.

Polisi walisema magenge yanayodaiwa kuwa na pinde na mishale yalivuka kutoka kaunti jirani na kuwashambulia wakaazi katika soko la Sondu na karibu na soko.

Magenge hayo yanadaiwa kuiba majumba pia.

Sondu ni mji mdogo wa mpaka kati ya kaunti za Kisumu na Kericho.

Mpaka kati ya kaunti za Kisumu na Kericho umekuwa na utata kwa miaka mingi huku mpaka wa awali ukidaiwa kuwa nyuma ya kituo cha Polisi cha Sondu kilichokuwa katika Kaunti ya Kisumu.

Mnamo 1992, mpaka ulirudishwa hadi Kaunti ya Kericho

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved