logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Niwakute!Pendeni maisha yenu,msishindane na vitu vya mitandao ya kijamii,'Akothee awaonya binti zake

Akothee amebarikiwa na wasichana 3 na amekuwa akiwapa ushauri na kuwashika mkono

image
na Radio Jambo

Burudani07 September 2021 - 11:36

Muhtasari


  • Akothee awaonya binti zake, kwa kuishi kulingana na maisha wanayoona mitandaoni

Kwa kweli wengi wanampenda msanii Akothee kwa ushauri wake kwa wasichana na akina mama na hasa kwa kusema ukweli.

Akothee amebarikiwa na wasichana 3 na amekuwa akiwapa ushauri na kuwashika mkono kila mahali.

Kupitia kwenye ukurasa wake wwa instagram msanii huyo aliwaambia binti zake wanapaswa kupenda maisha yao na kuacha maisha ya mitandao ya kijamii.

Akothee alipakia picha ambayo ilikuwa na ujumbe kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram kuzungumza na Wakenya na binti zake.

Kwa mujibu wa picha ilikuwa na ujumbe unaofuata;

"Kwa ushawishi wa watu wa mitandao ya kijamii unaendelea kuepuka uchangamfu Mtu huingia ulimwengu wa uongo

Kwa upande mmoja tamaa ya kupata vifaa kama vile magari ya anasa yanaweza kuwahamasisha na kwa upande mwingine inaweza kusababisha kuchanganyikiwa na unyogovu."

Akothe aliongeza maelezo chini ya picha ya kuonya binti zake  kamwe kujaribu kujisikia au kushindana na maisha ya watu kwenye mitandao ya ya kijamii.

"Kwa veshalia, rue.baby na  Makadia, kamwe jaribu kushindana au kupenda vitu kwenye mitandao ya  kijamii.

Unachoona sio juu ya ardhi, watu wana haribu maisha yao na madeni. Niwakute mnakosa kutumia kwa Vitu Haiwahusu.

Ninyi ni chini ya miaka ishirini na mitano. Jipeni wakati wa kukua. Acha mitandao ya kijamii peke yake "aliandika Akothee.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved