logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Davido na Chioma wachora tattoo za majina yao vidole vya pete

Wawili hao walimpoteza mwanao mwezi Novemba alipozama kwa bwawa la kuogelea nyumbani.

image
na Radio Jambo

Burudani15 January 2023 - 12:22

Muhtasari


Wawili hao walimpoteza mwanao mwezi Novemba alipozama kwa bwawa la kuogelea nyumbani.

Mwanamuziki wa Nigeria Davido na mkewe, Chioma Kila mmoja amechora tattoo ya mwenzake katika kidole cha pete.

Haya yanajiri wiki kadhaa baada ya kuripotiwa kufunga ndoa ya kitamaduni siku chache kufuatia kifo cha mwanao Ifeanyi aliyeripotiwa kuzama kwa bwawa la kuogelea nyumbani kwao Lagos.

Kulingana na ripoti katika vyombo vya habari vya Nigeria, ni watu wa karibu tu wa familia walioruhusiwa kuhudhuria hafla ya kufanya harusi ya kitamaduni, lakini bila simu zao za rununu.

Kipindi hicho ambacho kilikuwa kigumu sana kwa wawili hao, hakuna aliyedhubutu kuzungumza mitandaoni lakini blogu moja ilisema kuwa ni kweli harusi ya kitamaduni ilifanyika nyumbani kwa kina Davido ambapo mahari ya Chioma yalitolewa kwa ukamilifu.

Picha sasa ambazo zinasambazwa mitandaoni zinaonesha wawili hao kila mmoja akiwa na jina la mwenzake katika kidole cha pete, kama njia moja ya kuhakikishiana mapenzi yasiyojua kufa hata baada ya kufiwa na mwanao wa kipekee Novemba mwaka jana.

“Harusi ya kitamaduni ambayo ina watu wachache wa familia na marafiki waliohudhuria bila kamera kuruhusiwa ilifanyika katika Nyumba ya baba yake Davido na mahari ya Chioma ililipwa kikamilifu, hii inakuja baada ya Chioma kumwambia Davido kuwa hakuna kitu kingine chochote cha kuangalia kama yeye. mtoto wa kiume anayewaunganisha hayupo tena,” mwanablogu maarufu wa Nigeria, Gist Lover's Gram aliripoti kipindi hicho.

Mwanamuziki huyo baada ya kimya cha muda, alionekana hadharani wakati wa sherehe za kufunga kombe la dunia alipotumbuiza mubashara.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved