logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gengetone Haiwezi Maliza Mwaka Huu Kama Haijakufa Tena! – Miracle Baby

“Vijana wenye tulikuwa tunaimbia Gengetone kitambo sasa hivi ni watu wako na familia wanatafuta kazi. Hao watataka tuwaambie vitu vya kupata kazi, venye watapata pesa.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani11 February 2025 - 12:45

Muhtasari


  • Miracle Baby alisema kwamba kwa sasa yeye atasalia tu katika kuimba muziki wa Mugithi na kueneza injili, akitabiri Gengetone iliyofufuka kufariki tena kabla mwaka huu kuisha.
  • “Gengetone ilikuwa inaenda kumaliza vijana, ilikuwa inauwa watu, hivyo mimi siwezi rudi kwa kitu chenye kilikuwa kiniue,” Miracle Baby alisema.

Peter Miracle Baby, msanii wa Mugithi aikataa Gengetone

ALIYEKUWA msanii wa Gengetone, Peter Miracle Baby amefichua kwa nini hawezi rudi tena katika uimbaji na utunzi wa mirindimo hiyo.

Akizungumza kwenye podcasti ya Nguthii, Miracle Baby alisema kwamba Gengetone ilikuwa inaelekea kuua vijana na kusema kwamba yeye kama mmoja wa hao vijana, hawezi rudi katika ‘mauti’ hayo.

Miracle Baby alisema kwamba kwa sasa yeye atasalia tu katika kuimba muziki wa Mugithi na kueneza injili, akitabiri Gengetone iliyofufuka kufariki tena kabla mwaka huu kuisha.

“Gengetone ilikuwa inaenda kumaliza vijana, ilikuwa inauwa watu, hivyo mimi siwezi rudi kwa kitu chenye kilikuwa kiniue,” Miracle Baby alisema.

“Gengetone ilikuja kisha ikaisha, hivyo huwezi niambie nirudi kwa kitu chenye kilikuja na kisha kikaisha. Sikudanganyi, Gengetone haimalizi huu mwaka, haiwezi rudia. Hivyo kama hatutakuja na mkakati mwingine sioni kama kuna maana yoyote tunafanya katika hii sanaa,” aliongeza.

“Hatuwezi ishi place moja, baana joo tunazidi kuzeeka ..izo doba ziachiwe up coming wajijenge vile tu zilitujenga tusipo do ivo tutaishi na millions of views bt kwa mfuko zero...for now acha ni pige gospel mugithi zangu.”

Msanii huyo alisema kwamba Gengetone ilikuwa inatumia lugha chafu na haiwezi kudumu kwa muda mrefu kwa sababu watu waliokuwa wanaipenda kipindi kile sasa hivi wameshakomaa kiakili na hawataki tena kusikiliza kwa lugha chafu ambayo ilikuwa inatumika kwenye miziki hiyo.

“Vijana wenye tulikuwa tunaimbia Gengetone kitambo sasa hivi ni watu wako na familia wanatafuta kazi. Hao sasa si wenye tutakuwa tunaimbia, hao watataka tuwaambie vitu vya kupata kazi, venye watapata pesa. Lakini ukisema niimbe tena kuhusu makalio ina maana ninarudi kuimbia tena wenye wako kidato cha 4 sasa, hapo sasa nitakuwa naenda mbele ama narudi nyuma?” Miracle Baby alijieleza.

Miracle Baby alisema kwamba hadhira ya Gengetone ambayo ilikuwa inapenda miziki ya kuzungumzia makalio na viuno vya wanawake sasa ni watu wazima wanataka kusikiliza michongo ya kusaka hela na Imani ya kuishi kuiona kesho.

“Sasa hivi nimeamua kukwama kwa Mugithi na pia kama nitaimba hizo zingine haitakuwa Genge, nitakuja na muziki wangu kivyangu, muziki yenye mtu anaeza sikiliza impe motisha kwa maisha,” alisema.

Hii hapa video akizungumza;

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved