logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ringtone Ajitolea Kumpa Hifadhi Nyanyake Brian Chira Nyumbani Kwake Runda

“Nakukaribisha uje uishi na mimi hapa Runda. Nitakupatia ‘main house’ na mimi nitahamia ‘servant quarter’,” Ringtone alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani13 February 2025 - 11:37

Muhtasari


  • Aidha, Ringtone alimtahadharisha bibi huyo kuwa makini na vijana wa TikTok akidai kwamba wanamchezea na asingependa kuona wakiendelea kumfanyia shere. 
  • Tiktokers walikusanya zaidi ya milioni 8 pesa za Kenya mwezi Machi mwaka jana na kutumia sehemu yazo kumjengea bibi huyo nyumba 

Ringtone amtaka bibi yake Brian Chira kuishi kwake Runda

MWINJILISTI Ringtone Apoko amejitolea kumpa hifadhi nyanyake aliyekuwa TikToker, Brian Chira katika jumba lake la kifahari la mtaani Runda baada ya bibi huyo kusema kwamba anakoishi hakuna usalama wa kutosha.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ringtone alichapisha video akiwa mbele ya jumba lake barazani na kusema kwamba yuko tayari kuishi na bibi huyo huko Runda ambako kuna usalama wa kutosha.

Aidha, Ringtone alimtahadharisha bibi huyo kuwa makini na vijana wa TikTok akidai kwamba wanamchezea na asingependa kuona wakiendelea kumfanyia shere.

“Shosho wa Chira, hawa vijana wa TikTok wanakuchezea sana, mimi nakupenda. Sasa fanya hivi, kama mahali ile nyumba ulijengea na unaona hauna raha kule, nakukaribisha uje uishi na mimi hapa Runda. Nitakupatia ‘main house’ na mimi nitahamia ‘servant quarter’,” Ringtone alisema.

Tamko la msanii huyo aliyepata umaarufu zaidi ya miaka 15 iliyopita kupitia kibao cha ‘Pamela’ linakuja kipindi ambapo nyanyake Chira amekuwa katika majibizano makali ya tiktokers baada ya kudai kwamba anawazia kuuza nyumba waliyomjengea.

Tiktokers walikusanya zaidi ya milioni 8 pesa za Kenya mwezi Machi mwaka jana na kutumia sehemu yazo kumjengea bibi huyo nyumba kumuenzi Chira ambayo waliipa jina Chira Clan.

Hata hivyo, wiki mbili zilizopita, bibi huyo alijitokeza akisema kwamba eneo iliko hiyo nyumba si eneo salama na kusema kwamba anawazia kuiuza ili kuhamia sehemu salama zaidi.

Bibi huyo alisema kwamba kama TikTokers hawatomruhusu kuiuza nyumba, basi wanafaa kuketi chini kwa mara nyingine tena ili wamfikirie na usalama wake, akipendekeza kwamba itakuwa bora zaidi kama watamzungushia ua la umeme kwenye nyumba hiyo.

Tangu kipindi hicho cha moja kwa moja, bibi huyo amekuwa mada motomoto kwenye TikTok, huku wengi wakihoji kwa nini alionekana kukosa shukrani, huku wengine wakipendekeza kuwa kulikuwa na masuluhisho bora ya ukosefu wa usalama kuliko kudai nyumba mpya kabisa.

 

Mmoja wa wale waliomkosoa waziwazi ni msaidizi wake wa zamani, Baba Talisha, ambaye alimsuta kwa kile alichotaja kuwa kutokuwa na shukrani moja kwa moja kwa jamii ya TikTok ambayo ilikuwa imempitia.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved