logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Grand P: “Mlisema Eudoxie Yao sio size yangu, sasa mnasema nimeona mtoto, mnatakaje?”

“Wakati nilipost Jirani yangu (Eudoxie Yao), mliongea sana hadi mkachoka mkisema sio size yangu. Sasa nimepata ambaye ni size yangu na mumeleta kauli eti nimeoa mtoto.” Watu

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani23 February 2025 - 15:02

Muhtasari


  • Katika picha hiyo, alikuwa ameshikana na mpenzi wake mpya ambaye alimtambulisha siku ya wapendanao kwa jina Mariame Kaba.
  • Kijana huyo amekuwa katika miaka ya nyuma kwenye uhusiano na sosholaiti wa Ivory Coast Eudoxie Yao ambaye ana umbile kubwa maradufu kumliko Grand P.

Grand P na mpenzi mpya

MSANII kutoka Guinea, Grand P amelalamika baada ya kupokea kauli za kejeli kwamba mpenzi wake mpya nim toto sana kwake kutoka kwa wale waliokuwa wakimcheka kwamba mwanasosholaiti Eudoxie Yao hakuwa size yake.

Akipeleka kwenye ukurasa wake wa Facebook, Grand P alisema kwamba hajui watu wenye chuki huwa wanataka nini kwani wao ndio walikuwa wanamcheka kuwa Eudoxie Yao ni mkubwa sana kwake na sasa baada ya kupata wanayetoshana, bado watu wameibuka na kejeli kwamba ameoa mtoto.

“Ufike wakati mkome sasa watu wangu, wakati nilipost Jirani yangu (Eudoxie Yao), mliongea sana hadi mkachoka mkisema sio size yangu. Nilikubali ukosoaji wenu. Sasa nimepata ambaye ni size yangu na mumeleta kauli eti nimeoa mtoto. Watu wenye chuki sana nyinyi... kueni na siku njema,” Grand P alisema.

Katika picha hiyo, alikuwa ameshikana na mpenzi wake mpya ambaye alimtambulisha siku ya wapendanao kwa jina Mariame Kaba.

Kijana huyo amekuwa katika miaka ya nyuma kwenye uhusiano na sosholaiti wa Ivory Coast Eudoxie Yao ambaye ana umbile kubwa maradufu kumliko Grand P.

Uhusiano wake na Yao ulionekana kutumbukia mchangani mapema 2023 ambapio kufikia Aprili, alitangaza kuingia katika penzi la mwanadada mwingine aliyeitwa kwa jina Yubai Zhang.

Grand P alitangaza mahusiano yao kupitia akaunti yake ya Facebook akithibitisha mapenzi yake na mrembo huyo wa Kiasia na kuweka wazi kuwa hakuna nafasi ya watu wenye wivu maishani mwao.

"Yubai Zhang wangu, hakuna nafasi kwa watu wenye wivu," alisema chini ya picha zake na Zhang alizochapisha Facebook.

Balozi huyo wa Guinea nchini Mali alikatisha mahusiano yake na mwanamitindo Yao mwaka wa 2021 baada ya kuwa kwenye mahusiano na mwanamitindo huyo kwa takriban miaka mitatu.

Wawili hao walitangaza kukuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mwaka wa 2020 baada ya kuchapisha picha wakiwa pamoja.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved