

MSANII mashuhuri wa Dancehall, Adidja "Vybz Kartel" Palmer ameonesha majuto yake katika kujichubua rangi ya Ngozi yake ili kuonekana mweupe.
Msanii huyo mashuhuri alijadili historia
yake ya upaukaji wa ngozi wakati wa kuonekana hivi majuzi kwenye kipindi cha
redio cha Hot97 akiwa na mtangazaji wa redio wa Marekani Ebro Darden.
Akitafakari juu ya kipindi hicho cha maisha
yake, Kartel alisema kuwa siku za nyuma alikuwa anapaua Ngozi yake ili kufanya Ngozi
yake kuwa nyeupe ya kuwezesha kuonekana kwa tattoo zake.
"Namaanisha kwa mtazamo wa nyuma
hakika ilihusiana na kujipenda, lakini kwa upande mwingine nilipokuwa nikifanya
hivyo, akili yangu haikuniambia hivyo. Akili yangu ilikuwa ikiniambia
'ninafanya hivi ili kuonyesha tattoos zangu' ... nilichora tattoo nyingi.”
Kartel pia alisema wakati wa mahojiano
kwamba amepunguza tabia yake ya pombe na sigara na anatazamia kuoa mpenzi wake
Sidem Öztürk na kupata "watoto wa Kituruki".
Baada ya kuachiliwa huru kutoka jela
alikotumikia kifungo cha miaka 13, Kartel sasa anaamini kwamba maisha yake
yatabadilika kwa kiasi kikubwa kulingana na mikakati ambayo amejiwekea.
Kulingana na mambo haya, Kartel anaonekana
kubadilika, kwani nyimbo zake nyingi za awali zilikuwa na maudhui ya ngono ya
wazi na marejeleo ya matumizi mabaya ya dawa za kulevya, ambayo huenda yalikuwa
na athari mbaya kwa wafuasi wake wachanga duniani kote.
Uvumi ulipozuka kwamba Kartel ameanza
kuchubua rangi ya Ngozi yake takribani miaka 15 iliyopita, baadhi walidai
kwamba alikuwa anataka kuwa na muonekano kama wa Sean Paul ili kufanikiwa zaidi
katika muziki wa Dancehall.
Hayo ni kwa mujibu wa mtendaji mkuu wa
kampuni Zachary Harding, ambaye ni meneja wa zamani wa Sean Paul.
Katika makala iliyotuchapishwa kwenye
mtandao wa LoopTT mnamo 2020, aHarding alinukuliwa akisema: “Mimi na yeye
(Kartel) tulikuwa na mazungumzo marefu, na akaanza kuuliza ni jukumu gani ‘rangi
ya kahawia’ ya Ngozi ya Sean Paul ilichukua katika mafanikio yake na hii
ilikuwa sahihi wakati Kartel alipoanza kupauka.”
"Niliona kuwa ni ya kuvutia kwa
sababu alivutiwa na swali la 'je, rangi ya kahawia ya Sean ilikuwa sababu ya
ushawishi katika mafanikio yake' dhidi ya mafanikio ya Kartel," Harding aliendelea.
Ingawa Kartel amefanikiwa sana nchini
Jamaika na anachukuliwa kuwa Mfalme wa Dancehall, hajawahi kushinda Grammy au
kufurahia mafanikio ya kimataifa kama Sean Paul.


