logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto Ahakikishia Polisi Ulinzi Kamili Wakiwa Kazini

Alilaani ujasiri unaokua wa wahalifu waliowashambulia polisi siku za hivi karibuni, akionya kuwa vitendo hivyo havikubaliki na havitavumiliwa tena.

image
na Tony Mballa

Burudani28 June 2025 - 16:56

Muhtasari


  • Aidha, alitoa agizo kwa maafisa wa usalama kusimamia juhudi za amani na mshikamano katika maeneo yao, akisema wana jukumu si tu la kutekeleza sheria bali pia kuongoza juhudi za mshikamano wa kitaifa.
  • Kauli za Ruto zinakuja kufuatia matukio ya maafisa kushambuliwa na wahuni wakiwa kazini, ya hivi punde zaidi ikiwa ni wakati wa maandamano ya Jumatano.

Rais William katika hafla yard kuwakabithi hadhi wakuu wa jeshi
Rais William Ruto ameapa kukomesha vitisho dhidi ya maafisa wa polisi, akisisitiza kuwa usalama wao ni kipaumbele cha kitaifa.

Alisisitiza kuwa serikali ina wajibu wa kuwalinda wale wanaowalinda Wakenya.

Akizungumza Jumamosi katika Ikulu ya Nairobi alipokuwa mwenyeji wa maafisa wa usalama na wale wa Utawala wa Serikali ya Kitaifa kutoka kote nchini, Rais aliwahakikishia maafisa hao kuwa watapata ulinzi kamili wanapotekeleza majukumu yao.

“Kila afisa wa polisi anayehatarisha maisha yake kuwalinda watoto wetu, familia zetu, na taifa letu lazima ajue kuwa usalama wake umehakikishwa,” Ruto alisema.

“Wanapolitumikia taifa, serikali ya Kenya chini ya uongozi wangu itahakikisha familia zao na maisha yao pia yanalindwa.”

Alilaani ujasiri unaokua wa wahalifu waliowashambulia polisi siku za hivi karibuni, akionya kuwa vitendo hivyo havikubaliki na havitavumiliwa tena.

“Hatuwezi kuwa na nchi ambapo wahalifu wanawafukuza maafisa wa polisi. Kama maisha ya polisi yako hatarini, basi hakuna mtu aliye salama,” alitangaza.

Ruto alihakikishia kuwa maafisa hao watapewa vifaa vyote vinavyohitajika ili kutekeleza majukumu yao bila woga.

“Huwezi kuwalinda wengine ikiwa wewe mwenyewe huna usalama. Wanaume na wanawake wetu waliovaa sare lazima walindwe na wapewe uwezo wa kuwalinda wengine.”

maafisa wa usalama na wale wa Utawala wa Serikali ya Kitaifa kutoka kote nchini
Maafisa wa usalama na wale wa utawala

Aidha, alitoa agizo kwa maafisa wa usalama kusimamia juhudi za amani na mshikamano katika maeneo yao, akisema wana jukumu si tu la kutekeleza sheria bali pia kuongoza juhudi za mshikamano wa kitaifa.

Kauli za Ruto zinakuja kufuatia matukio ya maafisa kushambuliwa na wahuni wakiwa kazini, ya hivi punde zaidi ikiwa ni wakati wa maandamano ya Jumatano.

Maafisa kadhaa walishambuliwa jijini Nairobi.

Waliohudhuria kikao hicho walikuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen, Katibu wa Wizara Raymond Omollo, Mkurugenzi Mkuu wa DCI Mohamed Amin, na Naibu Makamishna Wakuu Gilbert Masengeli (APS) na Patrick Tito (KPS).

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved