logo

NOW ON AIR

Listen in Live

GARISSA: Maafisa Wa Usalama Wa Kenya Watibua Shambulizi La Al Shabaab

GARISSA: Maafisa Wa Usalama Wa Kenya Watibua Shambulizi La Al Shabaab

image
na

Dakia-udaku02 October 2020 - 16:10

Wanamgambo wa Al-Shabaab. | picha: the-star.co.ke

Maafisa wa usalama wa Kenya wametibua jaribio la wapiganaji wa Al Shabaab kushambulia kijiji kimoja huko Ijara katika kaunti ya Garissa kinachojulikana kama Yumbis.

Wapiganaji hao walijaribu kupeperusha bendera yao katika vijiji vya Yumbis na Welmarer kabla ya wenyeji kuwaarifu maafisa wa usalama.

Wanamgambo hao waliteka nyara vijiji hivyo Alhamisi jioni baada ya kuwazidi nguvu maafisa wa polisi wa utawala katika eneo hilo.

Hakuna yeyote aliyejeruhiwa katika shambulizi hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved