logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nakupeza sana,' Aliyekuwa muigizaji wa Machachari Baha amwandikia mamake ujumbe huu

'Nakupeza sana,' Aliyekuwa muigizaji wa Machachari Baha amwandikia mamake ujumbe huu

image
na

Habari05 October 2020 - 09:08
baha
Kumpoteza mama hasa ukiwa katika umri wa kati ni jambo ngumu sana na ambalo si rahisi kwa wengi hasa kama ni mwanafunzi masomo yake huwa yanakatizwa kwa muda huku wakimuomboleza mpendwa wao.

Aliyekuwa muigizaji wa machachri Tyler Kamau Mbaya almaarufu Baha kupitia kwenye mitandao ya kijamii ya instagram aliweza kumkumbuka mama yake ambaye alikuwa muigizaji wa humu nchini kwa ujumbe kuwa anampeza sana.

https://www.instagram.com/p/CF6uEJhDXUP/

Mama yake Baha alifahamika kama Beth Nyamura almaarufu Wanade katika kipindi cha mother-in-law ambacho hupeperushwa katika runinga ya Citizen.

Wanade alipoteza maisha yake mnamo mwaka wa 2013 baada ya kuugua saratani.

Baada ya kuposti picha ya mama yake aliandika ujumbe huu.

"Akina mama ni zawadi bora kutoka kwa Mungu, nakupeza sana." Aliandika Baha.

https://www.instagram.com/p/CF6x0AmDu9q/

Aliaga dunia muigizaji huyo akiwa katika kidato cha kwanza katika shule ya upili ya Nairobi, baada ya miaka miwili Baha na ndugu yake walimpoteza baba yao na kuwa yatima, tangu siku hiyo wawili hao wamekuwa wakitia bidii katika kazi zao na kushikana mkono kwa kila jambo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved