logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilikuwa nikiuza ‘herb’ ili kujikimu kimaisha. Asema mtangazaji wa Radio Jambo Mbusi

Mbusi pia amekana ripoti ambazo zimekuwa zikisambazwa  mitandaoni kwamba donge alilopewa kujiunga na Radio Jambo ni zito sana . Amesema pesa anazolipwa ni nyingi lakini sio kiasi ambacho hutajwa katika  ripoti hizo .

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku27 October 2020 - 09:59

Muhtasari


  •  Mbusi ana watoto watatu wa kike 
  •  Mtangazaji huyo wa Radio Jambo pia ni mwimbaji 
  •  Ametambulika kwa weledi wake wa lugha ya Sheng na kuwavutia vijana katika kipindi chake cha rege 

 

Mtangazaji maarufu wa Radio Jambo na  mfuasi mkubwa wa mtindo wa kirasta Mbusi  amesimulia safari yake katika fani ya usanii hadi kujipata katika redio .

 Mbusi ambaye  alikuwa akihojiwa na MC Jessy katika kipindi chake cha Youtube cha Jessy Junction amezua ucheshi sana kuhusu safari ya kujipinda ya maisha yake kuanzia alivyokuwa akifanya kazi ya kuigiza katika  National Theatre hadi alvyopata kazi  katrika kituo cha Gheto Radio . Amesimulia kwamba haikuwa rahisi kuingia redioni moja kwa  moja kwani  kuna wakati alilazimika kuuza ‘Mmea’ ambao anauita ‘Ngwelo’ ili kujikimu pamoja na familia yake kwani wakati huo mkewe alikuwa mja mzito

  Kinyume na wengi wanavyofikiri kwamba safari yake ya redioni ilikuwa rahisi Mbusi amesema kwamba kwa miaka miwili unusu alikuwa akifanya kazi ya utarishi ama Messenger  pale Gheto radio ambapo mshahara wake ulikuwa shilingi 3000 .

‘ Ningengoja kulipwa mwisho wa mwezi .lakini walikuwa wanasahau kama ninafaa kulipwa ….so ikifika tarehe 15 huko ndio nauliza malipo kisha mtu anaingia kwa mfuko yake ananipea  mshahahara wangu’ alisema Mbusi huku akimuacha na kicheko kizito Jessy ambaye hakuamini kwamba Mhusi aliyapitia yote hayo .

 Baada ya fursa kupatikaa Ghetto  Radio Mbusi amesema aliendelea kufanya kipindi na wenzake hadi fursa ya kuingia Radio Jambo ilipofika . Anasema hakuna yeyote aliyetaka kuhama naye kuja Radio Jambo na alipata tatizo sana wakati huo kumtambua mmoja wa wenzake ambaye angekuja naye katika kituo hicho cha Radio Africa .Baadaye ,amesema mwenzake Lion , ndiye aliyepiga moyo konde na kuamua kuhama naye kuja Radio Jambo na kuanzisha kipindi cha Mbusi na Lione Teke Teke . Mbusi pia amekana ripoti ambazo zimekuwa zikisambazwa  mitandaoni kwamba donge alilopewa kujiunga na Radio Jambo ni zito sana . Amesema pesa anazolipwa ni nyingi lakini sio kiasi ambacho hutajwa katika  ripoti hizo .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved