logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mtu akinitukana akinisema mimi nashukuru,'Diamond awajibu wanaotaka ang'atuliwe kwenye tuzo za BET

Staa huyo alisema kwamba mtu amseme wala amtukane hayo yote anashukuru.

image
na Radio Jambo

Habari15 June 2021 - 11:29

Muhtasari


  • Diamond awajibu wanaotaka ang'atuliwe kwenye tuzo za BET
  • Staa huyo alisema kwamba mtu amseme wala amtukane hayo yote anashukuru

Msanii wa Bongofleva, Diamond Platnumz amewajibu wanaotaka aondolewe kwenye tuzo za BET akisema ni mawazo yao na anayaheshimu.

Staa huyo alisema kwamba mtu amseme wala amtukane hayo yote anashukuru.

Akizungumza na runinga ya Wasafi msanii huyo alikwa na haya ya kusema;

“Mimi naheshimu mawazo ya kila mtu, mtu akinifurahia, akinitukana akinisema mimi nashukuru

“Epuka sana kumchukia mtu anayezungumza kitu kibaya juu yako, huwezi kujua kaamka kavurugwa hasira zake na kaamua kukumalizia wewe, kesho mwenyewe akikaa atajuta na kukuomba msamaha,” Diamond Alizungumza.

Pamoja na wasanii kumuunga mkono Diamond katika kile kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kumpigia kura katika tuzo za BET alizochaguliwa kushiriki, baadhi ya wadau wanaona hastahili kuungwa mkono.

Wadau hao wamemkemea waziwazi kupitia mitandao ya kijamii wakidai kuwa hajalitumia vema jina lake la msanii mkubwa kukemea maovu, badala yake amekuwa akifanya mambo yake binafsi.

Mapema mwaka huu Diamond alivuma sana mitandaoni baada ya kutoa kibao chake cha 'Waah' akimshirikisha msanii wa Rhumba Koffi Olomide.

Ni kibao ambacho kilivunja rekodi kwenye youtube baada ya kuokea watazamaji wengi kwa muda mfupi.

Hii hapa video ya mahojiano hayo;

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved