logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchekeshaji maarufu Nicholas Kioko alikuwa akitoboa wanawake masikio

Mchekeshaji maarufu wa Kikamba Nicholas Kioko alisimulia historia ya Maisha yake tangu alipokuwa mdogo.

image
na Evans Omoto

Mastaa wako17 April 2025 - 15:10

Muhtasari


  •  Baada ya hapo Nicholas  alikuja jiji kuu la Nairobi na kujiunga  na light academy wakati ambapo alihitimisha masomo yake ya kidato cha  nne.
  • Kulingana na maelezo ya Kioko alipata wakati mgumu alipokuwa akiendesha biashara hiyo  ni baada ya vijana fulani kuweza  kumfukuza  kutoka katikati ya jiji na kumwacha akiwa katika hali ngumu ya maisha.
Msanii Mchekeshaji

Mchekeshaji  maarufu wa Kikamaba Nicholas Kioko alisimulia historia ya  Maisha yake tangu alipokuwa mdogo.

 Nicholas Kioko alikuwa akihojiwa na kituo kimoja cha radio nchini wakati ambapo alisimulia usuli na  asili ya maisha yake. Kioko alizaliwa gatuzi la Machokos eneo bunge la Yatta, alijiunga  na shule  moja ya msingi na  kusoma  hadi shule ya upili katika kidato cha pili kabla ya kufukuzwa shuleni na mwalimu mkuu kwa  tuhuma  za utomvu wa nidhamu.

 Baada ya hapo Nicholas  alikuja jiji kuu la Nairobi na kujiunga  na light academy wakati ambapo alihitimisha masomo yake ya kidato cha  nne.

 Baada  ya  kutamatisha masomo yake Kioko aliazimia kuanza  biashara  ya  kuuza maji, peremende na biskuti katika barabara kuu za  kule Nairobi.

Kulingana na maelezo ya Kioko alipata wakati mgumu alipokuwa akiendesha biashara hiyo  ni baada ya vijana fulani kuweza  kumfukuza  kutoka katikati ya jiji na kumwacha akiwa katika hali ngumu ya maisha.

 Aliamua kwenda katika kituo kikuu cha mabasi cha Machakos mjini  Country Bus wakati ambapo aliendeleza biashara  hiyo ambapo alielezea kuwa alikuwa akipata riziki ya kila siku bila matata yoyote na kwa kuhakikisha kuwa yuko imara kimaaisha.

Baadaye  alipewa wazo na  rafiki yake mmoja aliyemwambia kuwa angependa  kumwonyesha jinsi ya kutoboa akina dada masikio ili kuongeza urembo na aweze kuwa anaitekeleza kazi hiyo wakati ambapo anahisi yuko sawa.

'' Baada ya kutoka mjini kwa barabara niliazimia kuja kwenye  kituo cha mabasi ya  kuenda Magharibi na Nyanza ili kurahihisha kazi yangu  nikiwa huko.

 Ninafurahia kwa sababu nilipata rafiki yangu mmoja aliyeazimia kunipa maarifa na ujuzi zaidi nikajifunza  jinsi ya kuwatoboa wasichana masikio na kuwapaka hina  kwa kucha zao. 

Hiyo kazi ilinisaidia pakubwa  sana na iliniwezesha kupata takribani shilingi 80,000 ambapo niliweza kufanikisha  ndoto yangu ya kusomea uanahabari katika chuo cha NBS.

Baada ya masomo ya NBS alienda masomo ya nyanjani  katika kituo cha Royal media ambapo alibahatika na kuwa msanii wa haiba wa kuchekesha watu baada ya kuandaliwa mkeka wa kukalia  na Lulu Hassan.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved