logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Picha) Simba anguruma Marekani! Diamond akutana na vigogo wa muziki duniani

Diamond pia amefichua kuwa amefanya muziki na Swae Lee wa kikundi cha Rae Sremmund

image
na Radio Jambo

Habari05 July 2021 - 08:56

Muhtasari


•Kupitia picha na video alizopakia kwenye mtandao wa Instagram, Diamond ambaye alienda Marekani kuhudhuria hafla ya kutuza wasanii ya BET Awards 2021 ameonekana akiburudika na wanamuziki wa nyimbo za kufoka waliobobea na kuheshimika kote duniani.

•Kwenye video moja ambayo Diamond alipakia kwenye akaunti yake ya Instagram mapema wiki iliyopita, Busta Rhymes alisikika akimuita Diamond 'Michael Jackson wa Afrika'

Diamond Platnumz na Wiz Khalifa

Mwanamuziki matata wa nyimbo za Bongo ameendelea kukutana na baadhi ya vigogo wa muziki nchini Marekani.

Kupitia picha na video alizopakia kwenye mtandao wa Instagram, Diamond ambaye alienda Marekani kuhudhuria hafla ya kutuza wasanii ya BET Awards 2021 ameonekana akiburudika na wanamuziki wa nyimbo za kufoka waliobobea na kuheshimika kote duniani.

Kati ya wasanii hao ni ikiwemo Busta Rhymes, OT Genasis, Wiz Khalifa, Akon, Hit Maka na Real Swizz (mtengenaji muziki).

Kwenye video moja ambayo Diamond alipakia kwenye akaunti yake ya Instagram mapema wiki iliyopita, Busta Rhymes alisikika akimuita Diamond 'Michael Jackson wa Afrika'

Inakadiriwa kuwa huenda mwanamuziki huyo ambaye aliibuka wa pili kwenye tuzo la BET kitengo cha International Act anatengeneza muziki na wasanii hao.

Diamond pia amefichua kuwa amefanya muziki na Swae Lee wa kikundi cha Rae Sremmund.

Rhymes ambaye anaheshimika sana kwenye sanaa ya muziki wa kufoka alisema kuwa  Diamond ni mwanamuziki 'hatari


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved