logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tafadhali niombeeni,'Nyashinski awaambia mashabiki baada ya kufichua amepata maambukizi ya koo

Kulingana na Nyashinski maambukizi hayo yalikuja kutokana na mazoezi makali kabla ya tukio hilo.

image
na Radio Jambo

Habari12 November 2021 - 12:00

Muhtasari


  • Kulingana na Nyashinski maambukizi hayo yalikuja kutokana na mazoezi makali kabla ya tukio hilo
Screenshot-from-2020-06-18-14_21_12

Rapa maarufu nchini Nyamari Ongegu, almaarufu Nyashinski, anasema anaweza kosa kuhudhuria  onyesho lake kwenye tamasha la 'Destination Africa Festival' ambalo muigizaji wa Nigeria Adekunle Gold ndiye msanii mgeni.

Nyashinski siku ya Ijumaa alisema amepata maambukizi ya koo ambayo yanatishia kupatikana kwake kutumbuiza kwenye onyesho hilo.

Kulingana na Nyashinski maambukizi hayo yalikuja kutokana na mazoezi makali kabla ya tukio hilo.

“Huyu anahitaji IMANI! Nimekuwa na wiki ya kusisimua na vipindi vikali vya mazoezi ya kujiandaa na tamasha za Destination Africa

Kwa bahati mbaya, jana nilipata maambukizi ambayo yameambukiza koo yangu ghafla na kutishia utendaji wangu,” aliandika Nyashinski kwenye hadithi zake za Instagram.

Rapa huyo, huku akiomba maombi kutoka kwa mashabiki wake, aliongeza kuwa anatarajia maonyesho mengine kwenye tamasha hilo.

"Tafadhali tafadhali niekeni kwa maombi yenu."

Kutoka kwetu wanajambo tunamtakia afueni ya haraka.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved