logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msijaribu! Najuta kufanya surgery - Munalove

Munalove amewaonya mashabiki na watanzania wote kuepuka kutaka kubadilisha sehemu za miili yao akisema kwamba anapitia kipindi kigumu tangu afanyiwe upasuaji huo.

image
na Radio Jambo

Habari07 February 2022 - 09:33

Muhtasari


• Msanii kutoka Tanzania, Munalove amesema kwamba anajuta kufanya upasuaji ili kujiongezea baadhi ya sehemu za mwili wake.

• Munalove amewaonya mashabiki na watanzania wote kuepuka kutaka kubadilisha sehemu za miili yao akisema kwamba anapitia kipindi kigumu tangu afanyiwe upasuaji huo.

Munalove100

Msanii kutoka Tanzania, Munalove amesema kwamba anajuta kufanya upasuaji ili kujiongezea baadhi ya sehemu za mwili wake.

Munalove amewaonya mashabiki na watanzania wote kuepuka kutaka kubadilisha sehemu za miili yao akisema kwamba anapitia kipindi kigumu tangu afanyiwe upasuaji huo.

Kupitia ujumbe aliochapisha katik ukurasa wake wa Instagram, Munalove ametoa ahadi kwa mashabiki wake kwamba karibuni atawaelezea aliyoyapitia tangu achukue hatua hiyo.

“Achananeni na surgery, msifanye ntakuja kuwaeleza vitu vingi ninavyopitia, nampenda sana Yesu,” aliandika Munalove.

Mwanadada huyo anaonekana kujutia kitendo hicho, jambo ambalo linaonekana kusambaratisha uhusiano wake na Mungu huku akitoa hakikisho kwamba amejirudi na sasa anampenda Yesu na kwamba atamtumikia daima.

Wasafi tv

Munalove ambaye mwaka jana alifanya upasuaji wa dimples na mwili wake kiujumla anasemekana kupitia kipindi kigumu cha madhara yaliyotokana na upasuaji huo , jambo ambalo limempelekea kutoa ushauri kwa mashabiki wake kutojaribu kufuata mkondo huo.

Kwa sasa mashabiki wanasubiri kusikia kutoka kwake kuhusu kile alichokipitia baada yake kufanya upasuaji ili kubadilisha sehemu zake za mwili.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved