logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mjadala waibuka baada ya Wema Sepetu kuomboleza kifo cha 'Kakake'

Alitumia instastori yake kueleza kuwa tetesi hizo zilikuwa ni uongo.

image
na

Habari17 February 2022 - 06:10

Muhtasari


• Wema Sepetu  amejitokeza na kueleza zaidi  kuhusu posti aliyochapisha jana kwenye ukurusa wake wa instagram akiomboleza kifo cha Kaka yake.

wema 5 (1)

Muigizaji wa Filamu za Bongo, Wema Sepetu  amejitokeza na kueleza zaidi  kuhusu posti aliyochapisha jana kwenye ukurusa wake wa instagram akiomboleza kifo cha Kaka yake.

Posti hiyo  ilitafsiriwa vibaya na baadhi ya wanamitandao nchini Tanzania huku tetesi zikiibuliwa kuwa alikuwa anazungumzia Pofesa Jay.

Wema ambaye ni mshindi wa Miss Tanzania 2006, kutokana tetesi hizo zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, Alitumia instastori yake kueleza kuwa kinachotafsiriwa kwenye posti ni uongo na kueleza kama ingekuwa ni Profesa Jay angetoa habari zaidi.

 

“Huyu ndio niliemaanisha jamani.. msinielewe  vibaya, ingekuwa vingine ningeandika habari zaidi,”alisema Wema Sepetu.

Profesa Jay amekuwa  Hospitalini  kwa takribani wiki nne, ambapo anaendelea kupokea matibabu. 

Serikali ya rais  Samia Suluhu iliahidi kugharamia matatibu ya Mwanamuziki Profesa Jay.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved