logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Spika wa bunge la Nairobi Benson Mutura kukesha katika seli za polisi

Mutura atalala katika kituo cha polisi cha Muthaiga akisubiri kufikishwa mahakamani.

image
na Radio Jambo

Habari21 April 2022 - 14:43

Muhtasari


• Siku ya Alhamisi alihojiwa kwa saa kadhaakatika makao makuu ya DCI kwa madai ya kumuibia muajiri wake kwa kuitisha marupurupu ya usafiri na ilhali hakusafiri.  

• Mutura aliandamana na wakili wake alipoelekea katika makao makuu ya DCI mwendo wa saa tano mchana na kuhojiwa kwa takriban saa tano. 

• Siku ya Jumatano Mutura alidai kwamba masaibu yake yalianza pale aliposema kwamba Nairobi Metropolitan Services ni taasisi haramu. 

Spika wa Bunge la Kaunti ya Nairobi Benson Mutura akiongoza kikao cha mawasilisho mnamo Oktoba 26, 2021 katika vyumba vya bunge. Picha: FI

 Spika wa bunge la kaunti ya Nairobi Benson Mutura atalazimika kukesha katika seli za polisi.  

Mutura ambaye anakabiliwa na tuhuma za wizi atalala katika kituo cha polisi cha Muthaiga akisubiri kufikishwa mahakamani.  

Siku ya Alhamisi alihojiwa kwa saa kadhaakatika makao makuu ya DCI kwa madai ya kumuibia muajiri wake kwa kuitisha marupurupu ya usafiri na ilhali hakusafiri.  

Pia anakabiliwa na kosa la kuchukuwa kitambulisho cha afisa mmoja wa polisi aliyekwenda kumkamata siku ya Jumatano katika jumba la City Hall. 

Mutura aliandamana na wakili wake alipoelekea katika makao makuu ya DCI mwendo wa saa tano mchana na kuhojiwa kwa takriban saa tano. 

Siku ya Jumatano Mutura alidai kwamba masaibu yake yalianza pale aliposema kwamba Nairobi Metropolitan Services ni taasisi haramu. 

"Kama ilivyo kwa sasa, NMs ni shirika lisilo halali kwani kuongezwa muda wake kuhudumu hakukufuata sheria," alibainisha. 

Mutura, ambaye ni mbunge wa zamani wa Makadara alidai kwamba hatua ya kuongeza muda wa NMS ilifaa kuidhinishwa na bunge la kaunti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved