logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pritty Vishy ajibu madai ya Stivo kuwa alitoka kimapenzi na wanaume zaidi ya 50

•Stivo alidai kwamba alifahamu kuwa Pritty Vishy hakuwa mwaminifu ila akaendelea kustahimili huku akimuomba abadili mienendo. •Vishy amesema Stivo alikosa kumwamini na angepatwa na wasiwasi mwingi kila baada ya kumuona akitembea na mwanaume yeyote barabarani.

image
na Radio Jambo

Habari13 June 2022 - 17:37

Muhtasari


•Stivo alidai kwamba alifahamu kuwa Pritty Vishy hakuwa mwaminifu ila akaendelea kustahimili huku akimuomba abadili mienendo.

•Vishy amesema Stivo alikosa kumwamini na angepatwa na wasiwasi mwingi kila baada ya kumuona akitembea na mwanaume yeyote barabarani.

Stivo Simple Boy na aliyekuwa mpenzi wake Pritty Vishy

Hatimaye Pritty Vishy amejibu madai ya aliyekuwa mpenziwe Stivo Simple Boy kuwa alitoka kimapenzi na zaidi ya wanaume 50 walipokuwa wanachumbiana.

Simple Boy akiwa katika mahojiano ya hivi majuzi alidai kuwa mpenzi huyo wake wa zamani alikuwa anamcheza mara kwa mara.

Alidai kwamba alifahamu kuwa Pritty Vishy hakuwa mwaminifu ila akaendelea kustahimili huku akimuomba abadili mienendo.

"Mimi nilinyamazia tu. Nilikuwa nikimwambia  kama ananipenda cha kweli awachane na hayo mambo yake. Nilimwambia akuwe na mtu mmoja ili tufunge ndoa. Lakini haeleweki jameni," Alisema katika mahojiano na Oga Obinna.

Vishy akijibu madai hayo amesema Stivo alikosa kumwamini na angepatwa na wasiwasi mwingi kila baada ya kumuona akitembea na mwanaume yeyote barabarani.

"Shida ya Stivo ata akiniona kwa barabara nikitembea na mjomba wangu jioni angekuja aniambie alisikia nilikuwa natembea na mwanaume. Nilishangaa kwani sifai kutembea na watu kwa sababu nachumbiana na yeye.Huyo ni mpenzi sumu," Vishy alisema katika mahojiano na Obinna.

Kipusa huyo mwenye umri wa miaka 20 alidai ikiwa Simple Boy alifahamu kuwa hakuwa mwaminifu basi angekatiza mahusiano yao.

Vishy hata hivyo alikiri kuwa alijihusisha kwenye mahusiano na wanaume kadhaa tajiri wenye umri mkubwa wanaojulikana kama 'wababaz'

Alifichua kuwa aliwahi kuchumbiana na 'mubabaz' mmoja mashuhuri ambaye alikutana naye katika harusi.

"Nilikutana naye harusini. Alikuwa MC," Alisema.

Aidha kipusa huyo alidai kuwa pia Stivo alikuwa anamcheza na wanadada kadhaa ambao alikuwa akitaniana nao kwenye simu.

"Jambo hilo hadi ilileta shida. Ilikuwa karibu tupigane. Ni kama alikuwa ananicheza. Mimi nilikuwa najua tulikuwa kwenye mahusiano lakini pia huko nje anachumbiana," Alisema.

Vishy ameshikilia kuwa hakuwahi kushiriki tendo na ndoa na Stivo wakati wa mahusiano yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved