logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani

Nchi zinazongoza kwa matumizi ya Kiswahili ni Tanzania, Kenya na Uganda.

image
na

Habari07 July 2022 - 05:35

Muhtasari


• Nchi za Afrika zinazofunza Kiswahili shuleni ni Kenya, Tanzania, Rwanda, Uganda, Somalia, Kongo DRC, Sudan Kusini, Afrika Kusini, Botswana, Ethiopia, Namibia, Malawi-Mozambique na Burundi.

Waziri wa Utalii Najib Balala kuongoza maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani.

Leo ni maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani.

Kenya ilijiunga rasmi na mataifa mengine barani Afrika yanozungumza lugha ya Kiswahili katika kuadhimisha siku ya Kimataifa ya Lugha ya Kiswahili.

Tarehe saba Julai ilitengwa kuwa siku rasmi ya kusherehekea lugha hiyo na Shirika la Umoja wa Mataifa mnamo Novemba Mwaka Jana.

Kiswahili ndio lugha ya pekee ya Kiafrika ambayo imetambulika na Umoja wa Mataifa.

 Waziri wa Utalii Najib  Balala, akiongoza maadhimisho ya sherehe hizo jijini Nairobi, aliwaagiza wakenya wajivunie umaarufu wa lugha ya Kiswahili kwa Kuizungumza  na kujifunza, kama ishara ya uzalendo kwa nchi ya Kenya.

Kiswahili kimeorodheshwa na majarida mbali mbali kama lugha inayokuwa kwa kasi mno kote duniani huku nchi kadhaa za Afrika Mashariki zikitangaza kutumia lugha hiyo kama lugha rasmi ya mataifa hayo.

Nchi zinazongoza kwa matumizi ya Kiswahili ni Tanzania, Kenya na Uganda.

Nchi za Afrika zinazofunza Kiswahili shuleni ni Kenya, Tanzania, Rwanda, Uganda, Somalia, Kongo DRC, Sudan Kusini, Afrika Kusini, Botswana, Ethiopia, Namibia, Malawi-Mozambique na Burundi.

Sherehe pia inafanyika mjini Mombasa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved