logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kina dada jifunze kutoka kwa mtindo wa nywele wa Margret Kenyatta na Rachael Ruto - Muthee Kiengei

“Kazi kwenu wanawake wale mnaangushwa na mawigi zingine mnakuna kuna na kalamu na kugonga gonga na ngumi kama mmefunga jicho moja ya kusikiza utamu wa mba.......Siri ndio hio hapa,”

image
na Radio Jambo

Habari13 September 2022 - 06:55

Muhtasari


• Shabiki wake mmoja alimwambia aanze na kumrekebisha mkewe ambaye kulingana na shabiki huyo anaweka mtindo wa dredi kichwani.

Muthee Kiengei awataka wanadada kujifunza kutoka mtindo wa nywele wa margret na rachael ruto

Mchekeshaji na mchungaji Muthee Kingei ameonekana kufurahishwa na jinsi mama wa taifa anayeondoka Margret Kenyatta na yule anayeingia Rachael Ruto wanavyojinadhisha haswa katika vichwa vyao.

Kiengei kupitia ukurasa wake wa Facebook, alipakia picha ya pamoja ya wawili hao wakiwa wanatembea kwa pamoja huku wakiwa wamejawa na tabasamu.

Mama Margret Kenyatta na mama Rachael Ruto wamejulikana kwa kunadhifisha vichwa vyao kwa nywele fupi pasi na vipodozi vyovyote kama mawigi na nywele za kubandika, mtindo ambao umekumbatiwa sana na wanawake wengi amabo wana dhana kwamba kuonekana wa kisasa lazima uwe ya mindo wa kusuka nywele wenye haiba ya kisasa.

Kiengei aliwapa changamoto wanawake kama hao na kuwataka kujifunza kutoka kwa maam hao wa taifa kwani licha ya cheo chao kikubwa katika uongozi wa taifa, bado wanajiweka katika mtindo wa nywele ulio wa kawaida kabisa.

“Kazi kwenu wanawake wale mnaangushwa na mawigi zingine mnakuna kuna na kalamu na kugonga gonga na ngumi kama mmefunga jicho moja ya kusikiza utamu wa mba.......Siri ndio hio hapa,” Muthee Kiengei aliandika huku akiwataka kuangalia picha hizo za Margret na Rachael.

Shabiki wake mmoja alimwambia aanze na kumrekebisha mkewe ambaye kulingana na shabiki huyo anaweka mtindo wa dredi kichwani na kumtaka Kiengei kuanza kutoka nyumbani kwamba.

Kwa utani, Kiengei alisema kwamba tayari ameshamnyoa kwa nguvu kwani kutoweka mtindo kama wa kina maam hao wa taifa ni kama kumzuia asiwe rais siku za mbeleni.

Nimemnyoa saa hii, anazuia nisikuwe rais kwa nini,” Kiengei alijibu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved