logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mazishi ya Malkia: Bendera zapandishwa huku kipindi cha maombolezo kikifika mwisho

Malkia alizikwa katika hafla binafsi huko Windsor Jumatatu jioni

image
na Radio Jambo

Habari21 September 2022 - 03:44

Muhtasari


•Bendera kwenye majengo ya serikali ya Uingereza kote ulimwenguni zimepandishwa tena kutoka nusu mlingoti.

•Bendera katika makazi ya kifalme zitasalia nusu mlingoti hadi tarehe 27 Septemba siku moja baada ya muda wao wa maombolezo kuisha.

Bendera kwenye majengo ya serikali ya Uingereza kote ulimwenguni zimepandishwa tena kutoka nusu mlingoti, huku kipindi cha maombolezo ya kitaifa kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II kikiwa kinakaribia kumalizika.

Malkia alizikwa katika hafla binafsi huko Windsor Jumatatu jioni, kufuatia mazishi ya serikali huko London na maandamano ya kijeshi kuelekea Windsor Castle.

Lakini Familia ya Kifalme itaendelea kuadhimisha wiki nyingine ya maombolezo. Washiriki wa familia ya kifalme hawatarajiwi kutekeleza majukumu yoyote ya umma kwa wakati huu.

Bendera katika makazi ya kifalme zitasalia nusu mlingoti hadi tarehe 27 Septemba siku moja baada ya muda wao wa maombolezo kuisha.

Kasri ya Buckingham imesema wafanyikazi wa nyumba ya kifalme, wawakilishi kwenye majukumu rasmi na wanajeshi waliojitolea kutekeleza majukumu ya sherehe pia watazingatia maombolezo yaliyoongezwa.

Operesheni ya kusafisha inaendelea baada ya mamia ya maelfu ya watu kote Uingereza kumiminika London kutazama mazishi ya Malkia.

Wasafishaji katika Baraza la Southwark kusini mwa London walifanya kazi kwa saa 24 zaidi wakati waombolezaji wakiwa kwenye foleni ya kutembea wakiondoa tani saba za takataka katika mchakato huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved