logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ninakushukuru! Duale amshukuru Rais Ruto baada ya kuteuliwa kuwa waziri wa ulinzi

Kiongozi huyo wa zamani wa wengi alisimulia jinsi alivyoanza safari yake na Rais.

image
na Radio Jambo

Habari27 September 2022 - 16:55

Muhtasari


  • Mbunge huyo alitajwa miongoni mwa mawaziri 22 waliopendekezwa na Rais William Ruto waliomwona anafaa kuongoza katika afisi hiyo

Mbunge wa Garissa Mjini Aden Duale hamemsshukuru rais Ruto baada ya kuteuliwa kuwa waziri wa Ulinzi katika baraza la mawaziri siku ya Jumanne.

Mbunge huyo alitajwa miongoni mwa mawaziri 22 waliopendekezwa na Rais William Ruto waliomwona anafaa kuongoza katika afisi hiyo.

"Asante bosi wangu, Rafiki yangu na Rais wangu William Ruto. Leo alasiri nilipokea habari za kuteuliwa kwangu kama waziri wa ulinzi ajaye kwa heshima, furaha na unyenyekevu," akasema.

"Kwa hakika nimenyenyekea kwa fursa ya kutumikia watu wa Kenya kama katibu wa baraza la mawaziri la Ulinzi. Ninakushukuru Rais wangu kwa imani yako katika uongozi wangu na kwa kunipa fursa hii adhimu."

Kiongozi huyo wa zamani wa wengi alisimulia jinsi alivyoanza safari yake na Rais.

"Hakika, njia zetu na wewe Mheshimiwa zilikutana mwaka wa 2007 na tangu wakati huo nyota zetu zimeng'aa zaidi na zaidi," alisema.

Duale alisema Ruto amemsaidia sana katika safari yake ya kisiasa na hawezi kumshukuru vya kutosha.

“Tulianza safari yetu ya kuwatumikia wananchi kwa pamoja mwaka 2007 na kupitia wewe Rais wangu niliteuliwa kuwa Waziri wa Mifugo katika Serikali Kuu ya Muungano,” alisema.

Duale amekuwa mfuasi mkuu na mshirika wa Rais kwa miaka mingi, sifa ambayo ilimfanya kuteuliwa kuwa Kiongozi wa Wengi wa Wengi katika utawala wa Jubilee mnamo 2013.

Hii ilikuwa baada ya chama cha URP cha Ruto kuungana na TNA cha Rais wa zamani Uhuru Kenyatta kuunda serikali mpya.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved