logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond, Mbosso waeleza cheni zao zilivyokatika jukwaani na kupelekwa Uingereza kutengenezwa

Mikufu yao ya   dhahabu yenye michoro ya vichwa vyao inatajwa kuwa za gharama mno

image
na

Habari02 November 2023 - 09:38

Muhtasari


•Diamond platnumz na Mbosso wamesimulia jinsi mikufu  yao yenye vito vya dhahabu ilikatika walipokuwa wakitumbuiza wafuasi wao.

•Diamond alidokeza kuwa mkufu wake ulisafirishwa hadi Uingereza kwa kituo kimoja ili kufanyiwa ukarabati  kurudisha sehemu iliyokatika.

Mastaa wa Bongo nchini Tanzania Diamond platnumz na Mbosso wamesimulia jinsi mikufu  yao yenye vito vya dhahabu ilikatika walipokuwa wakitumbuiza wafuasi wao.

Diamond Platnumzs kwa upande wake alisimulia,"Mkufu wangu ulikatika kipande  kimoja wakati nlipokuwa nikitubuiza wafuasi wangu kwa kuwa ni wa gharama niliweza kuagiza wenye ujuzi waniuganishie."

Msanii huyu alidokeza kuwa mkufu wake ulisafirishwa hadi Uingereza kwa kituo kimoja ili kufanyiwa ukarabati  kurudisha sehemu iliyokatika.

Nyota huyu wa Bongo alieleza kuwa mikufu yake ni ya gharama mno na kwa kawaida yeye huchagua maeneo ambayo atakayovaa wakati wa tamasha na ziara yake.

Kwa upande wa msanii Mbosso alieleza kuwa ,"Mkufu wangu wenye mchoro wa kichwa changu ambao umeundwa kwa dhahabu ulikatika ila nashukuru kwa kuwa nilitumana kwa kituo hicho hicho   Uingereza na ukarudishwa. "

Wawili hawa walisimulia  hayo walipokuwa kwenye mahojiano ya moja kwa moja ndani ya basi walimokuwa wakisafiria.

Mikufu hiyo ya  dhahabu yenye michoro ya vichwa vyao inatajwa kuwa za gharama mno. Kulingana na mmoja wa watangazaji wa wasafi media ambaye aliwahoji, zinagharimu zaidi ya millioni 45  za Kenya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved